Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Ndugai: Nilimchapa viboko mpinzani wangu
Habari za SiasaTangulizi

Spika Ndugai: Nilimchapa viboko mpinzani wangu

Job Ndugai akiwa jukwaani katika uchaguzi wa mwaka 2015. Picha ndogo Dk. Joseph Chilongani aliyechapwa viboko na Ndugai
Spread the love

SPIKA wa Bunge la Jamhuri, Job Ndugai, amekiri kumshambulia kwa fimbo Dk. Joseph Chilongani, ambaye aliyekuwa mmoja wa washindani wake wenye nguvu wakati wa kinyang’anyiro cha kuwania kuteuliwa kuwa mgombea ubunge ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Ndugai alitoa ushuhuda huo leo Alhamisi, bungeni mjini Dodoma, kufuatia kuibuka kwa mjadala mzito juu ya matumizi ya adhabu ya viboko kwa wanafunzi wa shule za msingi.

Alisema, suala la adhabu ya vikobo, ni muhimu sana kwa kuwa hata mimi niliwahi kumchapa mtu viboko na kwamba miongoni mwa makabila ya wamasai na Wagogo, kuchapa viboko ni suala la kawaida.”

Hata hivyo, kauli ya Spika Ndugai ya kutaka kuhalalisha viboko inapingana na kinachoonekana kwenye mkanda wa video, uliyonakiri tukio hilo.

Kwa mujibu wa mkanda wa video unamuonyesha Spika Ndugai akimshambulia Dk. Chilongani, kunaonekana baadhi ya wazee wa kabila la Kigogo, pamoja na akina baadhi ya wanawake, wakilalamikia kitendo hicho.

Aidha, ndani ya mkanda huo wa video, baadhi ya waliokuwapo walionekana kuhuzunishwa na tukio hilo, huku wengine wakimzuia Ndugai kumshambulia Dk. Chilongani.

Ndugai alimtuhumu Dk. Chilongani kumpiga picha, mara baada ya spika huyo wa Bunge kuanza kufanya vurugu kwenye mkutano wa kampeni wa kura ya maoni kwa kile alichodai kuwa mshindani wake alikuwa anampiga picha.

Katika mjadala huo wa bungeni, baadhi ya wabunge walipinga adhabu hiyo na kuitaka serikali kutafuta adhabu mbadala na kuacha suala la viboko kwa wazazi, huku wengine wakitaka iendelee ili wanafunzi wawe na nidhamu.

Akijibu kuhusu mjadala huo, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, alisema kuwa utoaji adhabu ya viboko kwa wanafunzi unalenga kuimarisha nidhamu hasa kwa watoto wasiofuata sheria.

Prof. Ndalichako amewataka walimu kutumia taratibu stahiki wanapotoa adhabu hiyo.

“Niongelee hili suala, suala la utoaji viboko lengo lake sio kuongeza ufaulu bali kurekebisha dosari zilizjitokeza, suala la adhabu hutolewa pale mtu anapokiuka taratibu.

“Nitumie fursa hii kuwashauri wanafunzi kutii sheria bila shuruti, pale inapokuwa na ulazima pindi mwananfunzi anapokiuka kutumia taratibu za adhabu zilizowekwa na akienda kinyume ataadhibiwa,” amesema Prof. Ndalichako.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!