Tuesday , 19 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Shule, Vyuo binafsi walalamikiwa rushwa ya ngono
Elimu

Shule, Vyuo binafsi walalamikiwa rushwa ya ngono

Naibu Waziri wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Elimu, Joseph Kakunda
Spread the love

SERIKALI imesema kuwa baadhi ya Mameneja, Wakurugenzi pamoja na wamiliki wa shule binafsi na vyuo wanalalamikiwa kwa vitendo vya rushwa ya ngono hasa wakati wa kutoa ajira kwa walimu hususani jinsia ya kike. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Wizara ya Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) Elimu, Joseph Kakunda alipokuwa akifunga mkutano wa Shilikisho la Wamiliki na Mameneja wa Shule na Vyuo visivyo vya Serikali (TAMONGSCO) uliofanyika kitaifa mjini hapa.

Kakunda amesema kwamba licha ya kuwa shule za binafsi pamoja na vyuo vinamchango mkubwa katika jamii pamoja na serikali kuzitambua lakini yapo maeneo yanayolalamikiwa ikiwa ni pamoja na masuala ya rushwa.

“Yapo maeneo ya rushwa hasa katika rushwa ya ngono ni jambo la aibu hata hivyo wanaume wengi ndio wanaoongoza kuomba rushwa ya ngono,wanawake wengi wa Afrika hasa wa Kitanzania wanajiheshimu sana hivyo wanaume igeni mfano wa wanawake wengi.

“Rushwa ya ngono imekuwa ikilalamikiwa hasa wakati wa kipindi cha uombaji wa ajira najua siyo shule zote wala vyuo vyote vya binasi lakini kwa baadhi ya wanaofanya hivyo wanatakiwa kuacha mara moja kwani ni aibu kuwepo kwa vitendo hivyo,” amesema Kakunda.

Akizungumzia kuwepo kwa shule binafsi Kakunda amesema kuwa wapo baadhi ya Mameneja na Wamiliki ambao wanaendesha shule hizo kama biashara kwa kutoza ada kubwa na kusababisha hata wale waliopakana na shule hizo kushindwa kujiunga na shule hizo kutokana na kiwango kikubwa cha ada.

Kutokana na hali hiyo amewataka mameneja na wamiliki kurudi katika mwongozo wa sera ya elimu na mazingira ya usawa na uwezeshaji na isiwe katika misingi ya kibiashara.

“Zipo shule zenye majina makubwa kalini watoto wa jirani na shule hizo hawasomi hapo, hata mameneja na wamiliki hawatembelei wazazi na kuwaelezea mikakati ya shule zao na bei za ada wanazotoza hata kuwashawishi kuwa wanaweza kutoa ada kwa awamu ngapi ili kuwashawishi wazazi hao kuwa na mwamko wa kusomesha watoto katika shule hizo,” amesema Kakunda.

Katika hatua nyngine hakusita kuzungumzia baadhi ya shule binafsi kushindwa kutoa mikataba ya ajira kwa watumishi wao ikiwa ni hatua moja wapo ya kutowaingiza katika mifuko ya jamii watumishi hao jambo ambalo amesema ni ukiukwaji wa misingi ya utoaji wa ajira.

Amesema kutokana na hatua hiyo serikali haitasita kuwachukulia hatua wamiliki na mameneja watote ambao watakiuka utoaji wa mikataba kwa watumishi wao ikiwa ni pamoja na kutowapa fursa ya kujiunga katika mifuko ya kijamii.

Kakunda pia amekemea baadhi ya shule pamoja na vyuo binafsi ambavyo vinajiendesha bila kuwa na bodi ikiwa ni pamoja ya kuwafukuza wanafunzi bila kufuata utaratibu alisema kuwa pia zipo ambazo hazifuhati mihura rasmi ya serikali jambo ambalo kiongozi huyo alisema kuwa halikubaliki.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

Elimu

Takukuru wambana Mwalimu mkuu, atema bungo

Spread the loveMwalimu Mkuu wa shule msingi Hanihani, kata ya Igunga wilayani...

error: Content is protected !!