MAHAKAMA ya Hakim Mkazi mkoani Dodoma imemuagiza naibu waziri wa utamaduni, Sanaa na michezo, Juliana Shonza, kufika mahakamani kwa “hiari kesho” Ijumaa, vinginevyo itatoa amri ya kukamatwa na kufikishwa mbele ya mahakama kwa nguvu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).
Agizo hilo limetolewa kufuatia Shonza kushindwa kufika mahakamani
kutoa ushahidi kwenye kesi ya jinai aliyoifungua dhidi ya mbunge mwenzake, Saed Kubenea.
Katika kesi hiyo Na.8 ya mwaka 2018, Kubenea anatuhumiwa kumshambulia Shonza kwa kinachoitwa, “kitu chenye bapa,” jambo ambalo amedai limemsababishia maumivu makali na kuteguka viongo.
Kubenea amekana madai hayo na kuongeza, “yote yaliyoelezwa yamesheheni siasa za maji taka.”
Leave a comment