Friday , 2 June 2023
Home Kitengo Michezo Wambura ashindwa rufaa, sasa kuburuzwa mahakamani
MichezoTangulizi

Wambura ashindwa rufaa, sasa kuburuzwa mahakamani

Michael Wambura, Aliyekuwa Makamu wa Rais wa TFF
Spread the love

KAMATI ya Rufaa za Maadili ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetupilia mbali rufaa ya aliyekuwa Makamu wa Rais wa TFF, Michael Wambura, hivyo adhabu aliyopewa na Kamati ya Maadili ya shirikisho hilo itaendelea. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Wambura alifungiwa kutojihusisha na kujishughulisha na masuala ya mpira wa miguu maisha yake yote na Kamati ya Maadili ya TFF kwa makosa matatu ikiwemo la kupokea au kuchukua fedha za shirikisho hilo kwa malipo ambayo hayakuwa halali.

Akisoma hukumu hiyo, Mwenyekiti wa Kamati ya Rufaa za Maadili ya TFF, Ebenezer Mshana amesema wamesikiliza pande zote mbili za mrufani na mjibu rufani na kuzitupilia mbali rufaa zote za Wambura kutokana na kutokuwa na hoja za msingi.

Mshana amesema rufaa ya Wambura iliyopelekwa mbele ya kamati yao haina mashiko hivyo wameridhia adhabu aliyopewa katika Kamati ya Maadili kama ilivyoamuliwa ya kufungiwa maisha kujihusisha na soka.

Pia Mshana ameshauri TFF kupeleka tuhuma zilizomtia hatiani Wambura zipelekwe katika vyombo husika ili hatua nyingine zaidi zichukuliwe.

Mshana amesema mawakili wa mrufani walijikita zaidi katika hoja za mteja wao kutopewa nafasi ya kusikilizwa lakini hawakuwa na hoja hata moja ya kupinga mashtaka yaliyomtia hatiani katika Kamati ya Maadili.

Makosa mengine yaliyomtia hatiani Wambura mbali na kuchukua fedha za TFF, ni kugushi barua alipwe fedha za kampuni ya Jeck System na kufanya vitendo vinavyoshusha hadhi ya shirikisho hilo.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!