Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali yaahidi kutoa ushirikiano kwa LHRC
Habari za Siasa

Serikali yaahidi kutoa ushirikiano kwa LHRC

Spread the love
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola, amesema Serikali itaendelea kutoa ushirikiano kwa kituo cha msaada wa Kisheria na haki za binadamu (LHRC), ili kulinda misingi ya demokrasia na haki za binadamu. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Lugola amesema hayo wakati wa uzinduzi wa ofisi ya kituo cha LHRC jijini Dodoma, ulioambatana na maadhimisho ya miaka 24 tangu kuanzishwa kwake.

Amesema Serikali inatambua harakati na mchango wa kituo hicho katika kulinda na kutetea haki za wanyonge, hivyo ni wajibu wa mamlaka husika ambayo ni msimamizi mkuu wa haki kuonyesha ushirikiano kwa vitendo.

“Yapo mambo mengi ambayo yanahitaji usaidizi katika nchi hasa masuala ya kisheria, na kwa kutambua juhudi za wadau wapigania haki ndio maana leo hii tupo hapa ili kutoa hamasa na kufikia lengo,” alisema Lugola.

Aidha ameongeza kuwa Serikali inatambua wajibu wake katika kulinda haki za binadamu, na kwamba ni lazima kuwajengea watanzania uwezo wa kutambua, kutetea na kulinda haki zao.

“Kwanini tunafanya hivyo, ni kwa sababu kupata haki za msingi ni wajibu wa kila raia ili mradi mtu huyo asivunje sheria na anafuata misingi ya Demokrasia kwa kuzingatia Utawala wa Sheria,” aliongeza Lugola

Awali akiongea katika ufunguzi wa ofisi hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa kituo  Cha Sheria na haki za binadamu (LHRC), Wakili Anna Henga, amesema ili kulinda haki za binadamu wanaunga mkono juhudi za serikali katika kutimiza azma ya Tanzania ya viwanda inayoendana na utawala bora.

Henga amesema pia wanafurahishwa na juhudi za Serikali katika kukemea na kuchukua hatua kwa baadhi ya viongozi wasiokuwa na weledi, ambao huchafua taswira ya utawala wa kisheria, ikiwemo kupungua kwa ajali za barabarani.

“Pamoja na uwajibikaji pia moja kati ya mafanikio tunayojivunia ni kupunguza ajali za barabarani kutokana na kubadilisha mitizamo hasi ya watumiaji wa barabara kwa kuwafundisha utii wa Sheria bila shurti,” amesema Henga.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa LHRC aliyemaliza muda wake Hellen Kijo Bisimba, amewataka wafanyakazi wa kituo hicho, kufanya kazi kwa weledi na kufuata misingi haki kwa kila mmoja bila kubagua.

“Malengo ya LHRC ni Pamoja na kuwafikia watanzania walioko pembezoni ambao hawajui namna ya kutafuta haki zao, hivyo ni lazima kufanya kazi kwa kufuata misingi na taratibu husika,” alisema  Bi. Hellen

Kituo cha msaada wa Kisheria na haki za binadamu (LHRC), kilianzishwa Septemba 25, 1995 lengo ikiwa ni kuwajengea uwezo Watanzania namna ya kulinda na kutetea haki zao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!