Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Serikali: Kuna viwanda vipya 3,000
Habari za Siasa

Serikali: Kuna viwanda vipya 3,000

Mwita Waitara
Spread the love

SERIKALI imeeleza kuwa, mpaka sasa kuna jumla ya viwanda vipya 3,000 tangu kuanza kwa kampeni ya ujenzi wa viwanda katika Serikali ya Awamu ya Tano. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo tarehe 12 Juni 2019 na Mwita Waitara, Naibu Waziri wa Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) wakati akijibu swali la nyongeza kutoka kwa Sophia Mwakagenda, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), Sophia Mwakagenda.

Mwakagenda alitaka kujua idadi ya viwanda vilivyojengwa tangu kuanza mkakati wa ujenzi wa viwanda 100 kila mkoa. Kwenye swali lake amedai, mkakati huo ulianzishwa kisiasa.

 Waitara amesema,  tayari kwenye mikoa serikali imetenga maeneo kwa ajili ya viwanda ambapo tayari 300 vimeishajengwa.

“Mkakati huu ni sehemu ya mikakati mbalimbali inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Tano, ili kujenga uchumi wa viwanda uliofungamanishwa na maendeleo ya watu,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!