Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa NEC yaamua rufaa 60, Jesca arejeshwa kumvaa Dk. Mwigulu
Habari za Siasa

NEC yaamua rufaa 60, Jesca arejeshwa kumvaa Dk. Mwigulu

Jesca Kishoa
Spread the love

TUME ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) nchini Tanzania, imemrejesha Jesca Kishoa kuwa mgombea ubunge Iramba Magharibi Mkoa wa Singida kupitia Chadema. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Jesca aliyekuwa mbunge wa viti maalum, atachuana na wagombea wa vyama vingine akiwemo Dk. Mwigulu Nchemba wa CCM.

Uamuzi uliotolewa jana Ijumaa tarehe 11 Septemba 2020 na Mkurugenzi wa Uchaguzi, Dk. Wilson Mahera ilisema tume hiyo ilizipitia, kuchambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 60 kati ya hizo, mbili za wabunge na 58 za udiwani.

          Soma zaidi:-

Dk. Mahera alisema, “imekubali rufaa moja na kumrejesha mgombea katika orodha ya wabunge. Rufaa hiyo ni kutoka jimbo la Iramba Magharibi.”

Ingawa taarifa hiyo ya Dk. Mahera kutomtaja jina la mgombea lakini Jecsa mwenyewe aliandika kwenye kwenye ukurasa wake wa Twitter akishukuru kwa uamuzi huo wa NEC.

“Nashukuru Mungu kwa hili, sasa kazi ni moja tu, kulikomboa jimbo la Iramba,” aliandika Jesca ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Baraza la Wanawake wa Chadema-Bara (Bawacha).

Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Dk. Wilson Mahera

Katika uamuzi mwingine, Dk. Mahera alisema Tume imekataa rufaa moja ya mgombea ubunge wa Iramba Magharibi ambaye uteuzi wake ulitenguliwa.

Dk. Mahera alisema, Tume ilizipitia, kuzichambua na kuzifanyia uamuzi rufaa 58 za madiwani kati ya hizo 34 imezikubali na kuwarejesha wagombea katika orodha ya wagombea udiwani huku ikizikataa rufaa 23 za wagombea.

Taarifa yote ya Dk. Mahera hii hapa chini;

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!