Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Nanenane Singida, Dodoma iwe endelevu – Waziri Jafo
Habari za Siasa

Nanenane Singida, Dodoma iwe endelevu – Waziri Jafo

Suleiman Jafo, Waziri wa Tamisemi
Spread the love

SELEMAN Jafo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), ametoa maagizo kwa wakuu wa mikoa ya Dodoma na Singida na halmashauri zote kuhakikisha, maonesho ya wakulima nanenane yanakuwa endelevu. Anaandika Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Jafo ametoa maagizo hayo wakati wa ufunguzi wa maonesho hayo yaliyofanyika kikanda katika viwanja vya nzuguni Jijini Dodoma tarehe 4 Agosti 2019.

Akifungua maonesho hayo Jafo alisema, maonesho hayo ni kwa lengo la kutoka elimu kwa wakulima, hivyo ni wajibu wa halmashauri zote kuhakikisha zinaendeleza maeneo hayo sambamba na kuwepo kwa afisa kilimo, ambaye atafanya mahali hapo kuwa sehemu ya kituo cha kazi.

“Natoa agizo sasa kuwa, maonesho ya nanenane yawe maonesho endelevu. Kumekuwe na tabia ya kuacha maeneo na kuyatelekeza na kufanya sehemu ya kusubiri ufike msimu mwingine ili muweze kulupana posho.

“Ni lazima kila halmashauri zote kuhakikisha zinaendeleza kilimo katika halmashauri husika na kumteua bwanashamba kukaa katika eneo husika kama sehemu ya kituo chake cha kazi, ili kutoa elimu bora kwa wakulima na wafugaji,” alisema.

Kuhusu utafiti Jafo alisema, ni wakati wa watafiti kuhakikisha wanafanya utafiti kwa mazao yote ikiwa ni pamoja na kufanya utafiti wa wanyama.

“Katika hali ya utunzaji wa mazingira, sasa natoa maelekezo badilisheni upandaji wa miti kama sehemu ya utunzaji wa mazingira badala ya kupanda miti ya ajabu, pandeni miti ya matunda ili kupunguza tatizo la utapia mlo,” alisema Jafo.

Dk. Binilith Mahenge, Mkoa wa Dodoma alisema, pamoja na kuwepo kwa maonesho hayo, bado kunachangamoto ya kutokuwepo kwa maelewano kati ya TASO na serikali kusimamia shughuli hizo, jambo ambalo linasababisha wadau kushindwa kuwekeza katika maonesho hayo.

Hata hivyo, anewahamasisha Watanzania hususani wakazi wa Dodoma kujiunga katika Bima ya Afya iliyoboreshwa.

Dk. Rehema Nchimbi, Mkuu wa Mkoa wa Singida alisema, nanenane imekuwa mkombozo kwa wakulima wa Singida kwa kuweza kulima kilimo cha kisasa pamoja na kuwa na jiji la nyuki la kitaifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!