Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CUF yampigia goti Rais Magufuli 
Habari za Siasa

CUF yampigia goti Rais Magufuli 

Spread the love

CHAMA Cha Wananchi (CUF), kinaugulia maumivi ya kutofanya mikutano ya kisiasa hasa muda huu kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa baadaye mwaka huu. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Maumivu hayo yameelezwa na Salvatory Magafu, Naibu Mkurugenzi wa Sheria na Haki za Binadamu wa chama hicho wakati akizunguza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam.

Magafu ameeleza kwamba katazo la mikutano ya hadhara lililotolewa na Rais John Magufuli, limeathiri shughuli za mikutano na kumwomba rais ambaye ndiye amiri jeshi mkuu asitishe katazo hilo.

“Huu ni muda muafaka wa kuruhusu mikutano,” amesema Magafu na kuongeza “uchaguzi wa serikali za mitaa ni muhimu.”

Ofisa huyo wa CUF ameeleza kuwa, katazo hilo linakwenda kinyume na Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977 na kinyume na matamko ya Umoja wa Afrika katika kutetea uhuru wa kueleza.

“… ni kinyume cha sheria nyingine za nchi hii na matamko ya Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika ambayo sisi kama nchi, wanachama tumesaini na kuridhia, tunamsihi Rais Magufuli kuruhusu wakati huu tuanze kufanya mikutano ya kisiasa,” amesema Magafu.

Hata hivyo, Magafu amesema Jaji Francis Mutungi ambaye ni Msajili wa Vyama vya Siasa nchini ameeleza kutokuwa na barua ya chama chochote cha siasa kulalamikia kutofanya mikutano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!