Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge CCM ahoji ahadi za serikali
Habari za Siasa

Mbunge CCM ahoji ahadi za serikali

Catherine Magige, Mbunge wa Viti Maalum (CCM)
Spread the love

CATHERINE Magige, Mbunge wa Viti Maalum (CCM) leo tarehe 16 Aprili 2019, ameitaka serikali kueleza ni lini itakamilisha ahadi zake ilizotoa kwa jamii? Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Akiuliza swali la nyongeza bungeni, Catherine amehoji ni lini serikali itaweza kukamilisha ahadi zake hususani katika ujenzi wa soko la Mto wa Mbu, Arusha.

“Serikali imekuwa ikitoa ahadi kwa ajili ya maendeleo ya wananchi, lakini ahadi hizo zimekuwa zikichelewa. Mfano ni ahadi ya ujenzi wa soko la mto wa mbu mkoani Arusha, je ni lini ahadi ya ujenzi wa soko itakamilika?” amehoji Catherine.

Awali katika swali la msingi la mbunge wa Segerea, Bonnah Kamol (CCM) alitaka kujua ni kwanini serikali isijenge soko kubwa mbadala linaloweza kufikiwa na wananchi wa Kata ya Kinyerezi, Bonyokwe, Segerea na kata nyingine.

Pia mbunge huyo alitaka kujua ni kwanini soko la Kinyerezi lililozinduliwa na Mwenge mwaka 2017, lisifunguliwe ili kutoa huduma kwa wananchi wanaolizunguka?

Akijibu maswali hayo Naibu Waziri was Nchi Ofisi ya Rais,TAMISEMI- Mwita Waitara amesema kuwa, serikali inatambua ahadi zake zote na itazitekeleza.

“Serikali inatambua ahadi zote na zitatekelezwa kuhusu ujenzi wa soko la mto wa mbu mkoani Arusha, kutokana na hali hiyo, fedha za ujenzi wa soko zipo ni pamoja na kutoa wataalamu wa ujenzi wa soko hilo,” amesema Mwita.

Mbali na hilo alisema kuwa halmashauri ya Manispaa ya Impala iliweka kipaumbele cha kutekeleza Mardi wa kimkakati wa ujenzi wa soko la kisutu utakao gharimu kiasi cha sh.bilioni 12.17 na hadi sasa mradi umepokea sh.bilioni 3.92 na ujenzi unaendelea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!