Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ACT-Wazalendo yaibomoa CUF Tanga kimya kimya
Habari za SiasaTangulizi

ACT-Wazalendo yaibomoa CUF Tanga kimya kimya

Spread the love

CHAMA cha Wananchi (CUF), kipo kwenye wakati mgumu baada ya ACT-Waalendo kuendelea kubomoa ngome zake. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Licha ya kauli tata kutoka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kwamba, kinaweza kufutwa, chama hicho kimeendelea kupokea waliokuwa wanachama wa CUF kwenye maeneo mbalimbali ya nchi.

Katika jiji la Tanga, Kata ya Duga mamia ya waliokuwa wanachama wa CUF wamechukua kadi za ACT-Wazalendo kwa madai ya kuchoshwa na mwenendo wa Prof. Ibrahim Lipumba, Mwenyekiti wa CUF-Taifa na viongozi wengine wa chama hicho.

“Simuelewi Prof. Lipumba na viongozi wenzake, lakini nimechoshwa na mwenendo wa CUF. Naamini katika demokrasia ndio maana najiunga na ACT-Wazalendo,” amesema Godfrey Simon baada ya kuchukua kati ya CUF.

Kutokana na kazi inayofanywa na waliokuwa viongozi wa CUF baada ya kujiunga na ACT-Wazalendo, Ismail Jussa, aliyekuwa kiongozi mwandamizi wa CUF ameandika kwenye ukursa wake wa twetter akiwapongeza viongozi hao kwa kazi ya usajili wa wanachama wapya kutoka CUF.

“Mpambanaji Rashid Jumbe Hamza akiwaongoza waliokuwa wanachama wa CUF wa Kata ya Duga, Mkoa wa Tanga kushusha tanga na kupandisha tanga ili safari iendelee. ACT-Wazalendo ndiyo habari ya mjini,” ameandika Jussa.

Ado Shaibu, Katibu Mwenezi na Mawasiliano ya Umma wa chama hicho ameuambia mtandao wa MwanaHALISI ONLINE kuwa, shughuli za chama hicho hazijakwamishwa na chochote na kwamba, uimara wa hali ya juu wa ACT-Wazalendo sasa unadhihiri.

“Tanga na maeneo mengine ya nchi kazi inaendelea kama ilivyopangwa, wanachama wanaendelea kujiunga. Wao wenyewe wamefurahia ACT-Wazalendo, wamefurahia Maalim Seif Sharif Hamad kuhamia chama hiki,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

error: Content is protected !!