Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia alia na ajira mpya za walimu
Habari za Siasa

Mbatia alia na ajira mpya za walimu

James Mbatia, Mbunge wa Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro (NCCR-Mageuzi)
Spread the love

JAMES Mbatia, Mbunge wa Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro (NCCR-Mageuzi), amesema kuwa tatizo la walimu nchini badoni kubwa sana kwa sasa tofauto na inavyoelezwa na serikali, anaandika Dany Tibason.

Mbatia amesema kuwa inashangaza kuona serikali ikishindwa kupangia walimu vituo vya kazi ilihali wilaya mbalimbali hapa nchini zina uhaba wa walimu, ambapo alieleza kwamba wilaya ya Vunjo pekee ina upungufu wa walimu 207.

Alitoa kauli hiyo bungeni wakati wa kipindi cha maswali na majibu kwa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia ambapo alihoji; “ni lini serikali itaweza kutatua tatizo la uhaba wa walimu ambalo linaonekana kuwa kero kubwa katika maeneo mbalimbali nchini.”

Wakati Mbatia akihoji kuhusu hilo, naye Suzan Lyimo, Mbunge wa Viti Maalum (Chadema), katika swali la nyongeza alitaka kujua ni lini serikali serikali itaweza kufanya mgawanyo sawa wa walimu kwani walimu wengi wapo mijini wakati vijijini kuna upungufu mkubwa wa walimu.

Awali Doto Biteko, Mbunge wa jimbo la Bukombe (CCM), alitaka kujua ni lini serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha ili kuondoa upungufu uliopo katika wilaya ya Bukombe.

“Wilaya ya Bukombe ina mahitaji ya walimu wa shule za Msingi 1,425 ,kwani waliopo ni 982 na kuna upungufu wa 443.

“Je ni lini serikali itapeleka walimu wa shule za msingi wa kutosha ili kuondoa upungufu uliopo?” alihoji Biteko.

Akijibu maswali hayo ya Biteko, Mbatia na Lyimo, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI George Simbachawene alisema kwa sasa TAMISEMI imekuwa ikifanya utaratibu wa kupeleka walimu katika maeneo mbalimbali ambako kuna uhaba wa walimu.

“Tunawapangia walimu vituo vya kazi lakini wengi wanahama katika vituo vyao vya kazi kutokana na kutomudu hali ya miundombinu iliyopo katika sehemu husika ikiwa ni pamoja na halmashauri kushindwa kuwapatia motisha,” amesema Simbachawene.

Selemani Jafo, Naibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais –TAMISEMI, akitoa majibu ya nyongeza alisema, “Serikali inatambua upungufu wa walimu uliopo nchini ambapo mahitaji ya walimu wa shule za msingi na sekondari kwani waliopo ni walimu 188,481 na upungufu ni walimu 47,151.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!