Saturday , 10 June 2023
Home Kitengo Michezo Bocco aitwa Sauzi kumrithi Mbaraka
Michezo

Bocco aitwa Sauzi kumrithi Mbaraka

John Bocco
Spread the love

KOCHA Mkuu wa timu ya Taifa Tanzania, Salum Mayanga amemuongeza kwenye kikosi straika wa Simba, John Bocco kuchukua nafasi ya Mbaraka Yussuf aliyekuwa majeruhi, anaandika Catherine Kayombo.

Bocco ameshafika Afrika Kusini kujiunga na wenzake ambao wanatarajiwa kesho kushuka uwanjani kucheza mchezo wao wa Nusu Fainali ya michuano ya Baraza la Vyama vya Michezo Kusini mwa Afrika (Cosafa) dhidi ya Zambia.

Mshambuliaji huyo anachukua nafasi ya Mbaraka ambaye alipata majeruhi katika moja ya michezo yao ya awali ya kundi A, ambapo walikuwa pamoja na timu za Malawi, Mauritius na Angola.

Mayanga amesema amemuongeza Bocco katika kikosi hicho kwa malengo mawili, moja ni kujaza nafasi hiyo, lakini pia kuongeza nguvu kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Rwanda wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la Mataifa Afrika kwa wachezaji wanaochezea ligi za ndani (CHAN) zitakazofanyika mwakani nchini Kenya.

Mchezo huo unatarajiwa kufanyika Julai 15, mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza na marudiano yatafanyika mwishoni mwa mwezi au mwanzoni mwa Agosti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

MichezoTangulizi

Benki ya NBC yakabidhi kombe la ubingwa wa ligi kuu kwa Yanga

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa ligi ya NBC, Benki ya Taifa ya...

HabariMichezo

Benki ya NBC yazindua kombe jipya la Ligi Kuu Tanzania Bara

Spread the loveMDHAMINI Mkuu wa Ligi ya NBC , Benki ya Taifa...

MichezoTangulizi

Yanga malizeni ugomvi na Fei Toto – Rais Samia

Spread the love  RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

Michezo

Samia aipongeza klabu ya Yanga kwa hatua iliyofikia

Spread the love RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia...

error: Content is protected !!