Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Matokeo ya Kidato cha Sita haya hapa
Elimu

Matokeo ya Kidato cha Sita haya hapa

Wanafunzi wa kidato cha sita walipokuwa wanafanya mtihani
Spread the love

BARAZA la Mitihani la Taifa Tanzania (Necta) limetangaza matokeo ya kidato cha sita ya mwaka 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akitangaza matokeo hayo, Katibu Mtendaji wa Necta Zanzibar, Dk. Charles Msonde amesema ufaulu kwa mwaka huo umeongezeka kutoka 97.58% hadi kufikia 98.32% mwaka 2019 ikiwa ni sawa 0.74%. 

Amesema kuwa mtihani watahiniwa 91,298 walisajiliwa wakiwamo wasichana 37,948 ambao ni sawa na 41.56% na wavulana 53,350 sawa na 58.44% ambapo kati ya watahiniwa waliosajiliwa, watahiniwa wa shule walikuwa 80,216 na watahiniwa wa kujitegemea walikuwa ni 11, 082.

“Kati ya watahiniwa 91,298 waliosajiliwa kufanya mtihani , watahiniwa 90,001 sawa na asilimia 98.58 walifanya mtihani na watahiniwa 1,297 sawa na asilimia 1.42 hawakufanya mtihani huo kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za ugonjwa na utoro, watahiniwa wa shule, kati ya watahiniwa 80,216 waliosajiliwa, watahiniwa 79,770 sawa na asilimia 99,44 walifanya  mtihani ambapo wasichana walikuwa 33,883 sawa na asilimia 99.57 na wavulana 45,887 sawa asilimia  99.35. Watahiniwa 446 sawa na asilimia 0.56 hawakufanya mtihani,” amesema.

KUANGALIA MATOKEO YOTE INGIA HAPA

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

ElimuHabari za Siasa

MbungeCCM ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the love  MBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze...

ElimuHabari za Siasa

Walimu 52,551 kupandishwa madaraja mwaka huu

Spread the loveNaibu Waziri wa nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala...

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

error: Content is protected !!