Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Madiwani Manyoni wapigwa msasa
Habari za Siasa

Madiwani Manyoni wapigwa msasa

Geoffrey Mwambe, Mkuu wa Wilaya ya Manyoni
Spread the love

MADIWANI 28 toka Kata 19 za Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni wamepatiwa mafunzo maalum ya Uongozi, Maadili na Utawala Bora, Mafunzo, anaandika Dany Tibason.

Mafunzo hayo ya siku mbili yameanza Aprili 5 hadi 6 Aprili, mwaka huu katika Ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni kwa lengo la kuwajengea uwezo.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni, Geoffrey Mwambe akifungua mafunzo hayo amewataka madiwani kuyatumia mafunzo hayo ili yawasaidie katika kusimamia vyema sheria, taratibu na kanuni za utawala bora.

Katika mafunzo hayo pia aliwataka madiwani kujenga ushawishi kwa wananchi katika kushiriki kikamilifu shughuli za maendeleo wilayani humo.

“Mafunzo haya yamekuja wakati muafaka kwani kumekuwa na baadhi ya waheshimiwa madiwani kutojua mipaka ya utendajikazi wao na kupelekea migongano baina yao na watendaji wa vijiji ndani ya kata wanazozisimamia.

“Hivyo kupitia mafunzo haya, ninaimani yatawasaidia kujua mipaka ya utendaji kazi wao hivyo kwenda kushirikiana vyema na watendaji wa kata na vijiji katika maeneo yaokusimamia shughuli za maendeleo,” amesema Mwambe.

Muwezeshaji wa mafunzo hayo, Stella Saasita ambaye ni mchumi toka Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo na mbinu za ushawishi madiwani hao, ili kuleta mpokeo chanya kwa wananchi katika utekelezaji wa shughuli mbalimbali za kuwaletea maendeleo wananchi hususani miradi ya maendeleo.

Wakati huo huo, Madiwani walioshiriki mafunzo hayo yaliyoandaliwa na Halmashauri ya Wilaya ya Manyoni, wamepongeza uongozi wa halmashauri kwa kuandaa mafunzo hayo ambayo wameyataja kuwa yenye tija katika kuwaongezea uwezo.

Madiwani hao wamesema mafunzo ambayo wanayapata yatawafanya kuchochea zaidi shughuli za maendeleo katika kata zao pamoja na halmashauri kwa ujumla.

Mbali na hilo kwa pamoja madiwani hao wamesema mafunzo hayo yatawafanya kukua mipaka yao ya kazi na kuondokana na migongano kati ya madiwani na watendaji.

Hata hivyo madiwani wamesema kutokana na mafunzo hayo watawahamasisha wananchi kuchangia shughuliza za maendeleo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!