Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mwenyekiti CUF agoma kuondoka madarakani
Habari za Siasa

Mwenyekiti CUF agoma kuondoka madarakani

Christina Mdeme, Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini
Spread the love

LICHA ya Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Christina Mdeme kutangaza kumsimamisha uongozi wa Mwenyekiti wa mtaa wa Malimwa Kusini, Ismail Seifu (CUF), ametangaza kutokabidhi ofisi ya mtaa kama alivyoagizwa na DC, anaandika Dany Tibason.

Seifu amesema kitendo cha mkuu wa wilaya kumsimamisha nafasi hiyo haina maana yoyote na hatambui suala hilo kwani yeye alichaguliwa na waananchi na siyo mkuu wa wilaya.

Mkuu wa wilaya aliitisha mkutano wa adhara kwa maelezo kuwa wananchi walimpelekea tuhuma tano ambazo zilikuwa zikimkabili mwenyekiti huyo jambo ambalo amesema siyo tuhuma za wananchi bali ni tuhuma za kutengenezwa kamati yake ya utendaji ambao aliwasimamisha.

Akizungumza na waandishi wa habari Seifu, amesema licha ya mkuu wa wilaya kufanya utenguzi wa uongozi wake bado hatambui jambo hilo kwani waotakiwa kumwondoa ni wananchi waliompigia kura.

Seifu amesema wakati wa uongozi wake alihakikisha anapambana katika kukwamua maendeleo huku akiwa ameokoa zaidi ya Sh milioni nne za mradi wa mpango wa kunusuru kaya masikini TASAF ambazo zilikuwa zikilipwa katika kaya hewa zaidi ya kumi.

Awali kabla ya kusimamishwa uongozi kwa kutangaziwa tuhuma tano zilizomkabili Seifu amesema katika uongozi wake hakupendezwa na tabia ya baadhi ya viongozi kukwamisha maendeleo.

Mwenyekiti huyo amesema kuwa inasikitishwa na tabia ya viongozi hao kukwamisha maendeleo ya mtaa huo kwa kutosikiliza matatizo ambayo wanapelekewa.

Amesema licha ya kujitahidi kuhakikisha mtaa huo unapata maendeleo makubwa lakini bado kuna mambo ambayo viongozi wa Manispaa na wilaya wanashindwa kuyatolea maamuzi.

Seifu amesema analazimika kusema hivyo kutokana na kuomba wakaguzi wa milioni kumi ambao ulifanyika huku kukiwa na mapungufu ambayo yanatakiwa kufanyiwa kazi.

Mwenyekiti huyo amesema mbali na kuomba wakaguzi lakini bado ameweza kuokoa kiasi cha Sh. milioni nne ambazo zilikuwa zikitolewa katika kaya masikini kwa ajili ya kutekeleza mradi wa kaya masikini.

Amesema katika uongozi uliopita zaidi ya kaya kumi katika mtaa wa Mlimwa Kusini zilikuwa kaya hewa ambazo zilikuwa zikipokea mradi wa TASAF na taarifa hizo zipo katika ofisi ya mkuu wa wilaya ya Dodoma pamoja na ofisi ya Mkurugenzi wa Manispaa lakini hakuna hatua zozote zilizochukuliwa.

“Mtaa wa Mlimwa kusini hunaongozwa na mwenyekiti kutoka katika muungano wa vyama vinavyounda Ukawa kupitia CUF ambapo mtaa huo ni makazi ya Waziri Mkuu.

“Wapo wanasiasa ambao wamekuwa hawataki maendeleo na badala yake wanaingiza mambo ya siasa katika kazi, mtaa huu unaongozwa na CUF lakini wapo watu ambao wanatamani kuangusha utawala uliopo,” amesema mwenyekiti huyo.

Kwa upande wao viongozi wa Manispaa pamoja na wilaya hawakuweza kutoa ufafanuzi wa jambo lolote kuhusiana na alichokisema mwenyekiti huyo.

Hata hivyo ofisi ya Mkuu wa Wilaya ilimwandikia barua Kumb.Na.AB.380/507/01/17 ya kumtaka mkurugenzi wa Manispaa ya Dodoma kutoa taarifa ya ukaguzi uliofanyika katika mtaa wa Mlimwa Kusini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!