Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kuapishwa mrithi wa Lissu: Wapinzani wasusa, Ndugai apiga kijembe
Habari za SiasaTangulizi

Kuapishwa mrithi wa Lissu: Wapinzani wasusa, Ndugai apiga kijembe

Miraji Mtaturu akiapishwa rasmi kuwa Mbunge wa Singida Mashariki
Spread the love

MIRAJI Mtaturu ameapishwa rasmi kuwa Mbunge wa Singida Mashariki, akirithi mikoba ya Tundu Lissu aliyevuliwa ubunge wa Jimbo hilo. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Lissu alivuliwa ubunge kwa madai ya utoro na kutojaza  fomu ya maadili ya umma.

Mtaturu ameapishwa leo tarehe 3 Septemba 2019 bungeni jijini Dodoma, siku moja baada ya Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kukataa ombi la Lissu la kuutaka mhimili huo kuzuia kuapishwa kwake, hadi pale shauri lake kuhusu kuvuliwa ubunge litakapotolewa uamuzi.

Mbele ya Bunge, Mtaturu alikula kiapo cha uaminifu, huku wabunge wa upinzani isipokuwa wa Chama cha Wananchi (CUF) wakisusia zoezi hilo kwa kutohudhuria bungeni.

Baada ya Mtaturu kuapa, Spika wa Bunge, Job Ndugai amewaomba wabunge wamkaribishe Mtaturu huku akieleza kwamba wananchi wa Jimbo la Singida Mashariki wamepata mwakilishi halali bungeni.

“Kwa niaba yenu naomba tumkaribishe Miratji Mtaturu, Mbunge wa Singida Mashariki, sasa wananchi wa Singida Mashariki wanaye muwakilishi halali bungeni,” amesema Spika Ndugai.

Mnamo tarehe 28 Juni 2019 wakati akihitimisha mkutano wa kumi na tano wa Bunge, Spika Ndugai alitoa taarifa ya Lissu kuvuliwa ubunge Singida Mashariki.

Lakini tarehe 7 Agosti 2019 Lissu alifungua shauri Na. 18 la mwaka 2019 dhidi ya  Spika wa Bunge na Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) la kupinga kuvuliwa ubunge katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam kwa hati ya dharula.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!