Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi ya Mdee kumtusi Magufuli yapigwa kalenda
Habari za Siasa

Kesi ya Mdee kumtusi Magufuli yapigwa kalenda

Halima Mdee (mwenye nguo nyeupe) akiwa mahakamani akisubiri kesi yake kutajwa kabla ya kuhairishwa
Spread the love

KESI inayomkabili mbunge wa Kawe, Halima Mdee (Chadema), imepigwa kalenda hadi Oktoba 11,mwaka huu itakapoanza kusikilizwa, anaandika Hellen Sisya.

Mdee ambaye pia ni Mwenyekiti wa Baraza la Wanawake wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), anakabiliwa na kesi ya kutoa lugha ya matusi dhidi ya Rais John Magufuli.

Anadaiwa kutoa maneno hayo mwezi July mwaka huu, akiwa katika makao makuu ya chama hicho yaliyopo katika mtaa wa Ufipa, Kinondoni jijini Dar es salaam.

Kesi hiyo inasikilizwa na Hakimu Victoria Nongwa wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini Dar es Salaam na anatetewa na mawakili watatu wakiongozwa na Wakili msomi Peter Kibatala huku upande wa Jamhuri ukiwakilishwa na mawakili wawili wakiongozwa na wakili msomi, Mutalemwa Kishenyi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!