Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi kupinga matokeo ya urais: Tanzania yapewa siku 45 kujitetea  
Habari za Siasa

Kesi kupinga matokeo ya urais: Tanzania yapewa siku 45 kujitetea  

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepewa siku 45 na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu  (ACHPR) kupeleka majibu yake katika kesi iliyofunguliwa na Wakili Msomi, Jebra Kambole ya kupinga matokeo ya urais kutopingwa mahakamani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa barua iliyotolewa  tarehe 14 Februari 2019 na ACHPR na kusainiwa na Msajili wa mahakama hiyo, Dk. Robert Eno, zikipita siku 45 pasipo serikali kuepeleka majibu yake, Mahakama itaendelea na usikilizaji wa kesi hiyo.

Wakili Kambole aliifungua Kesi hiyo Na. 018/2018 mwaka jana dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiitaka Mahakama ya Afrika ipitie ibara ya 41 (7) ya katiba ya nchi ambayo imenyima mamlaka mahakama yoyote ile,  kuchunguza matokeo ya urais yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Katika hoja zake, Wakili Kambole anadai kuwa, ibara hiyo inakiuka Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!