Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kesi kupinga matokeo ya urais: Tanzania yapewa siku 45 kujitetea  
Habari za Siasa

Kesi kupinga matokeo ya urais: Tanzania yapewa siku 45 kujitetea  

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

SERIKALI ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imepewa siku 45 na Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu  (ACHPR) kupeleka majibu yake katika kesi iliyofunguliwa na Wakili Msomi, Jebra Kambole ya kupinga matokeo ya urais kutopingwa mahakamani. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa barua iliyotolewa  tarehe 14 Februari 2019 na ACHPR na kusainiwa na Msajili wa mahakama hiyo, Dk. Robert Eno, zikipita siku 45 pasipo serikali kuepeleka majibu yake, Mahakama itaendelea na usikilizaji wa kesi hiyo.

Wakili Kambole aliifungua Kesi hiyo Na. 018/2018 mwaka jana dhidi ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, akiitaka Mahakama ya Afrika ipitie ibara ya 41 (7) ya katiba ya nchi ambayo imenyima mamlaka mahakama yoyote ile,  kuchunguza matokeo ya urais yaliyotangazwa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Katika hoja zake, Wakili Kambole anadai kuwa, ibara hiyo inakiuka Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!