Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa JPM amewataka Watanzania kuvumiliana
Habari za Siasa

JPM amewataka Watanzania kuvumiliana

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS John Magufuli, rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewataka Watanzania kuwa na mioyo ya kuvumiliana, anaandika Hellen Sisya.

Rais Magufuli ameyasema hayo mapema leo hii akiwa katika ziara ya kikazi mkoani Singida na kusisitiza kuwa kila mmoja anatakiwa kuilinda amani.

“Niwaombe Watanzania, tuwe na mioyo ya kuvumiliana, tuitunze amani yetu.” alisema Rais Magufuli.

Aidha, Rais Magufuli amesisitiza kuwa suala la kulinda amani ni kila mmoja wetu na kuwataka watanzania kila mmoja kuwa mlinzi wa mwenzake.

Kauli ya Rais Magufuli imekuja wakati ambao viongozi wa kisiasa wa kambi ya upinzani wakikamatwa mara kwa mara kwa madai ya kutoa lugha za uchochezi, hatua inayoonyesha kuwa bado hakuna uvumilivu wa kisiasa hapa nchini.

Rais Magufuli amekuwa katika ziara ya kikazi kwa siku kadhaa sasa akitembelea mikoa mbalimbali ikiwemo Kigoma, Tabora na leo ndiyo alikuwa anahitimisha ziara hizo mkoani Singida.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!