Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Deni la taifa lazidi kupaa
Habari za Siasa

Deni la taifa lazidi kupaa

Spread the love

KAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imewasilisha taarifa ya mwaka kuhusu utekelezaji wa majukumu yake katika kipindi cha Januari, 2018 hadi Januari 2019 huku ikionesha kuongezeka kwa deni la taifa. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Aidha kamati hiyo imebaini kukua kwa deni la taifa likijumuisha fedha zilizokopwa na serikali kutoka katika vyanzo vya ndani na nje pia na sekta binafsi kutoka nje ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maendeleo.

Akiwasilisha taarifa ya Kamati ya Bunge leo 2 Februari 2019 bungeni jijini Dodoma, mwenyekiti wa kamati hiyo, George Simbachawene amesema, hadi kufikia Novemba 2018 deni la taifa limeendelea kukua taratibu hadi kufikia Sh 61.8 trilioni.

Pamoja na hayo amesema, ukuaji wa deni hilo umetokana na mahitaji ya uwekezaji kwenye miradi ya maendeleo na kijamii nchini kwa ajili ya kukuza uchumi.

“Kamati inashauri serikali kuangalia uwiano uliopo kati ya mwenendo wa upatikanaji wa mapato ya ndani pamoja na ulipaji wa deni la serikali na athari zake katika bajeti na uchumi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!