Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Balozi CCM akamatwa na bangi
Habari za SiasaTangulizi

Balozi CCM akamatwa na bangi

Viroba vilivyosheheni bangi
Spread the love

BALOZI wa nyumba kumi mkazi wa Kasumulu wilayani Kyela mkoa wa Mbeya, Andende Smoke Mbalwa (35) pamoja na Rose Charles (40) wanashikiliwa na Jeshi la Polisi mkoani humo kutokana na tuhuma za kukutwa na debe tatu za bangi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa za tukio hilo zimetolewa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, SACP, Ulrich Matei, ambapo amesema watuhumiwa hao walinaswa katika operesheni iliyofanywa na jeshi hilo.

Kamanda Matei amedai kuwa, Mbalwa na Charles ni wauzaji na watumiaji wa bangi hiyo. Na kwamba upelelezi dhidi yao unaendelea na watafikishwa mahakamani mara baada ya kukamilika.

Katika hatua nyingie, Kamanda Matei amesema Polisi wanawashikilia watu watatu, Okoka Sanga (48) mkazi wa Ushirika Tukuyu, Festo Hassan (25) na Cosmas Ngondo (33) mkazi wa kijiji cha Lema wilayani Kyela, kwa tuhuma za kumjeruhi kwa kumchoma kisu sehemu za shingoni Elizabeth Mwampamba (44) mkazi wa Stamiko.

“Inadaiwa kuwa mnamo tarehe 1Oktoba 2018 majira ya saa 00:05 usiku huko Kijiji cha Stamiko kilichopo Kata ya Busale, Tarafa ya Ntebela, Wilaya ya Kyela, Mkoa wa Mbeya. Elizabeth Mwampamba akiwa amelala nyumbani kwake ambapo anaishi na watoto wake, alivamiwa na mtu/watu wasiofahamika na kisha kuchomwa kisu sehemu za shingoni,” amesema Kamanda Matei.

Kamanda Matei amesema Mhanga wa tukio hilo amelazwa Hospitali ya Rufaa Mbeya kwa matibabu. Wakati polisi wakiendelea na upelelezi kubaini chanzo cha tukio hilo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!