Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto atilia shaka utekelezaji ripoti kikosi kazi, ataka Serikali itoe ratiba
Habari za Siasa

Zitto atilia shaka utekelezaji ripoti kikosi kazi, ataka Serikali itoe ratiba

Zitto Kabwe, Kiongozi wa ACT-Wazalendo
Spread the love

 

KIONGOZI Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, ameitaka Serikali itoe ratiba ya utekelezaji wa mapendekezo ya Kikosi cha Rais Samia Suluhu Hassan dhidi ya marekebisho ya mfumo wa demokrasia ya vyama vya vingi, akidai kuna juhudi za kuchelewesha mageuzi yake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Kiongozi huyo wa ACT-Wazalendo, ametoa wito huo leo Alhamisi, tarehe 24 Novemba 2022,akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam, ikiwa imepita mwezi mmoja tangu kikosi kazi hicho kikabidhi ripoti yake kwa Rais Samia.

“Tunaitaka Serikali iweke ratiba ya utekelezaji wa mapendekezo ya kikosi kazi ili tuweke mazingira mazuri ya siasa ya nchi yetu tuondoe manung’uniko ya wananchi katika mfumo mzima wa siasa ya nchi yetu, ili Uchaguzi wa Serikali za Mitaa wa 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025 zifanyike kwenye mazingira huru,” amesema Zitto.

Mwanasiasa huyo amesema “tuna wasiwasi kwamba kuna juhudi za kuchelewesha mageuzi haya ili tufike kwenye uchaguzi kukiwa na mazingira yale yale tuliyokuwa nayo 2019 na 2020. Mazingira ya watu kukatwa na kuenguliwa kwenye uteuzi, kugeuza shughuli ya uchaguzi kuwa shughuli ya kipolisi. Tunaona dalili hizo sababu hatuoni shughuli zikifanyika.”

Aidha, Zitto ameishauri Serikali iondoe malalamiko na manung’uniko ya baadhi ya wananchi hususan wanachama wa vyama vya siasa vya upinzani, wanaodai kufanyiwa vitisho na baadhi ya viongozi wa Serikali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!