Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto amwibua Mbwa wa Lugola
Habari za Siasa

Zitto amwibua Mbwa wa Lugola

Spread the love

SIKU moja baada ya Zitto Kabwe, kumweleza Kangi Lugola, Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi kwamba, ashughulike na mbwa wa polisi, hatimaye majibu yamepatikana leo alipo mbwa huyo. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Jana Julai 30, 2018 wakati akijibu agizo la kujisalimisha kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi mkoani Lindi kwa tuhuma za uchochezi, Zitto alisema kuwa haendi na mwisho wa taarifa yake kwenye ukyrasa wake wa twetter aliandika “…Nashauri Waziri ampate kwanza yule Mbwa wa Polisi Bandari.”

Leo mbwa huyo wa kazi maalum za Bandari ya Dar es Salaam aliyedaiwa kutoweka katika mazingira ya kutatanisha, anatakwa kupelekwa alikuwa kwenye mafunzo katika Bwalo la Polisi.

Kauli hiyo imetolewa na Msemaji wa Jeshi la Polisi, Barnabas Mwakalukwa katika mkutano na wanahabari.

Amezungumza hayo huku ukumbini hapo kukiwa na mbwa wawili wa polisi, akiwamo anayedaiwa kutoweka.

Amesema kulikuwa na mkanganyiko na hakuna mbwa aliyepotea.

“Tunataka kuwaambia kuwa, mbwa huyo alikuwa kwenye mafunzo ya Bwalo la Polisi na mbwa aliyekuwa hayupo siyo hobi,” amesema Mwakalukwa na kuongeza:

“Mbwa wote wapo hakuna hata mmoja aliyetoweka huwa wanaenda kwenye kazi na kurudi.”

Julai mwaka huu, Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola alimpa saa saba Mkuu wa Jeshi la Polisi, (IGP) Simon Sirro kuhakikisha mbwa huyo anarudi bandarini baada ya kupotea katika mazingira ya kutatanisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!