Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto aibuka na mbinu ya kuing’oa CCM
Habari za SiasaTangulizi

Zitto aibuka na mbinu ya kuing’oa CCM

Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo Zitto Kabwe aeleza mbinu zitakazotumiwa na chama hicho kukiondoa madarakani  Chama Cha Mapinduzi (CCM) kupitia uchaguzi wa serikali za mitaa na  uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza katika ufunguzi wa Mkutano wa Halmashauri kuu ya chama hicho leo tarehe 29, Septemba 2019, amesema kuwa Serikali ya CCM kwa kipindi cha miaka minne hakikukidhi matakwa ya wananchi hususani katika  uchumi.

“Uchaguzi wowote huhusu mambo ambayo yapo juu …unahusu mambo ambayo yapo chini wao wakija juu na ndege zao nyie nendeni chini na njaa za wananchi ambayo imesababishwa na sera za CCM.

“Wakija juu na Reli zao nyie nende chini na hali ya elimu katika maeneo yao wakija juu na ‘stieglers gorge’ nyie nendeni chini kuangalia maelfu ya vijana ambao hawana ajira wanateseka wakija juu la lolote lao nyie angalie yanayowagusa wanachi moja kwa moja,” amesema Zitto.

 Amesema kuwa ni watanzania wachache wanaoamini katika maendeleo ya vitu baadala ya watu kwa kuwa watu hawawezi kufanya shughuli za uchumi.

“Ni asilimia tano pekee ya  Watanzania wanaopanda ndege acheni wapigiwe kura na hiyo asilimia tano …hata hiyo tano hawatakuwa nayo yote mimi napanda ndege na sitawapigia kura,” anesema Zitto.

Amewataka wanachama wa chama hiko kuwaendea wananchi na kuwapigania juu ya masuala yanayogusa maisha yao moja kwa moja ndipo watakapoeleweka.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!