Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Watuhumiwa 467 uhujumu uchumi waomba toba, kulipa Bil. 107.1
Habari za SiasaTangulizi

Watuhumiwa 467 uhujumu uchumi waomba toba, kulipa Bil. 107.1

Biswalo Mganga, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mashtaka Tanzania (DPP)
Spread the love

WATUHUMIWA 467 wa uhujumu wameomba toba, na kukubali kurejesha serikalini fedha walizotafuna zaidi ya Sh. 107.1 bilioni. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Hayo amesema Biswalo Mganga, Mkurugenzi wa Mashtaka Nchini (DPP), leo tarehe 30 Septemba 2019, Ikulu Jijini Dar es Salaam, wakati akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa ushauri alioutoa Rais John Magufuli hivi karibuni, wa kuwasamehe watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kutubu na kurejesha fedha na mali.

DPP Mganga ameeleza kuwa, baadhi ya washtakiwa hao wako tayari kulipa Sh. 13.6 bilioni muda wowote kuanzia sasa, wakati wengine wameomba kulipa kwa awamu kiasi cha Sh. 94.2 bilioni.

“Katika kundi hilo, watu ambao wako tayari kurudisha moja kwa moja fedha jumla ni  Sh. 13.6 bilioni,” amesema DPP Mganga na kuongeza.

“Kundi la pili wako tayari kulipa kwa awamu, jumla yake Sh.  94.2 bilioni. Wako tayari kurudisha, wanasema watalipa kidogo kidogo. Ukijumlisha zote kwa wasthakiwa 467,  jumla ya fedha washtakiwa wa hujumu wako tayari kurudisha ni Sh.  107.1 bilioni.”

Hata hivyo, DPP Mganga amesema kuna baadhi ya watuhumiwa walishafuata taratibu za kisheria na kulipa mahakamani zaidi ya Sh. 1.40 bilioni, siku ya Ijumaa iliyopita.

“Ijumaa iliyopita kuna mtu mmoja alikubali kuitikia wito, alikiri mahakamani. Alikuwa andaiwa dola laki 4.5 alikubali kulipa pale pale. Thamani yake ni Sh. 1.3 bilioni, bado alilipishwa faini ya Sh. 5 milioni mahakamani.

“Ijumaa hiyo hiyo, kuna mtu alikuwa na gram 2123.64 za madini ya vito, yenye thamani ya Sh. 36.5 milioni, huyu alikiri na akalipa hizo fedha na madini hayo yakataifishwa,” amesema DPP Mganga.

Tarehe 22 Septemba 2019, Rais Magufuli alitoa mapendekezo kwa DPP Mganga, ya kutoa msamaha kwa watuhumiwa wa uhujumu uchumi walio tayari kuomba toba na kurejesha fedha au mali walizofisadi, ndani ya siku saba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!