Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Zitto afungua kesi kupinga muswada, yahairishwa mpaka mchana
Habari za SiasaTangulizi

Zitto afungua kesi kupinga muswada, yahairishwa mpaka mchana

Spread the love

KIONGOZI wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe na wenzake wawili, Joran Bashange na Salim Bimani wamefungua kesi Mahakama Kuu ya Tanzania kupinga Muswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa imehairishwa hadi leo saa nane mchana. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Kesi hiyo imefunguliwa leo katika Mahakama Kuu dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupingaMuswada wa Marekebisho ya Sheria ya Vyama vya Siasa na kuzuia usijadiliwe bungeni mpaka kesi ya msingi itakaposikilizwa.

Kwa mujibu wa Ado Shaibu, Katibu wa Itikadi, Mawasiliano na Uenezi, ACT Wazalendo, kesi hiyo imehairishwa mpaka saa nane ambapo Mahakama Kuu itaamua kuhusu hoja kuu mbili zilizozua ubishani mkubwa wa hoja baina ya upande wa wanasheria wa waombaji (Applicants) na upande wa Mwanasheria Mkuu wa serikali.

Hoja zilizoibua mvutano ni upande wa muda wa Mwanasheria Mkuu wa serikali kujibu hoja zilizoibuliwa na waombaji uongezwe kama ilivyoombwa na upande wa AG au upunguzwe kama ilivyoombwa na upande wa waombaji.

Pia kama Mahakama iweke zuio (Injunction) la kuzuia muswada kujadiliwa Bungeni, kama ilivyoombwa na waombaji mpaka kesi ya msingi itaposikilizwa na kuamuliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!