Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wajasiriamali waanika kinachoua VICOBA
Habari Mchanganyiko

Wajasiriamali waanika kinachoua VICOBA

Spread the love

WAJASIRIAMALI wilaya ya Temeke mkoa wa Dar es Salaam, wameeleza sababu zinazopelekea vikundi vya kuweka akiba na kukopa mikopo kufa na kuacha maumivu kwa wanachama walioweka fedha zao. Anaripoti Mwandishi Wetu  … (endelea).

Akizungumza katika mkutano wake na wanachama wa vikundi vya VICOBA Endelevu wilayani humo, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Temeke, Johari Mkonde amesema miongoni mwa sababu za vikundi hivyo kufa ni pamoja na usimamizi mbovu kuhusu masuala ya fedha na ukiukiwaji wa katiba za vyama hivyo.

Johari ambaye pia ni Mratibu wa Taasisi ya VICOBA Endelevu-SDA, amesema kitendo cha baadhi ya wanachama kutolipa mikopo yao kwa wakati na wengine kukimbia na fedha za vikundi, ni miongoni mwa sababu za vikundi hivyo kutotimiza malengo yake na hatimaye kuvunjika.

“Ulipaji wa mikopo umekuwa changamoto kubwa. Wasimamizi wa mikopo wanatakiwa kutowalea wanaogoma kulipa mikopo kwa wakati, inatakiwa wahakikishe waliokopa wanalipa madeni yao kwa wakati ili hizo fedha ziwanufaishe wanachama wengine,” amesema na kuongeza Johari.

“Kikundi kikishirikiana katika kufuatilia ulipaji wa madeni, wanaokopa hawawezi kukimbia na pesa, inatakiwa tuwe na msimamo ili tuweze kufikia malengo ya kujikwamua kiuchumi. Wale wanaohusika na marejesho waendelee na majukumu yao.”

Katika hatua nyingine, Johari amewahimiza wajasiriamali kusajili vikundi vyao vya kuweka akiba na kukopa mikopo serikalini, ili viweze kutambulika na kupata fursa zinapojitokeza

Johari ameeleza kwamba, changamoto ya wajasiriamali kutosajili serikalini vikundi vyao, imepelekea kutotambulika pindi fursa zinapojitokeza, na kuwataka wanachama wa vikundi hivyo kufuata taratibu na masharti ya usajili, ili wasajili vikundi vyao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!