Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari Waziri Ummy: Ma DED njooni na CV, kitambulisho
HabariHabari Mchanganyiko

Waziri Ummy: Ma DED njooni na CV, kitambulisho

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu
Spread the love

 

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais-Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Ummy Mwalimu amewataka wakurugenzi (DED) wapya 69 walioteuliwa kufika makao makuu ya ofisi hizo, Dodoma kesho Alhamisi, tarehe 5 Agosti 2021. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kati ya wakurugenzi hao watendaji 184 wa Halmashauri za Jiji, Manispaa,Miji na Wilaya waliteuliwa tarehe 1 Agosti 2021 na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, 69 ni wapya.

Miongoni mwa walioteuliwa ni wanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambao baadhi walijitosa kwenye uchaguzi ndani ya chama hicho kuwania ubunge wa majimbo ama viti maalum kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2020.

Wakurugenzi hao wanatakiwa kufika ofisini hapo saa 3:00 asubuhi, wakiwa na vyeti vya kuzaliwa, kitambulisho Nida, wasifu binafsi (CV), vyeti vya kitaaluma pamoja na picha mbili (passport size).

“Wakurugenzi ambao wahehamishwa vituo na wale walioendelea kuwepo kwenye vituo vyao vya awali waendelee na utaratibu wa kwenda kuripoti kwenye vituo vyao vya kazi kwa ajili ya makabidhiano kuanzia tarehe 3 Agosti 2021,” imeeleza taarifa ya Tamisemi iliyotolewa na Nteghenjwa Hoseah, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa ofisi hiyo

Taarifa hiyo imesema, wakurugenzi ambao uteuzi wao umesitishwa “wakaripoti kwa makatibu tawala mikoa yao mara moja.”

Mmoja wa waliowahi kuwa watumishi wa umma aliyeomba hifadhi ya jina lake amezungumzia taarifa hiyo ya Waziri Ummy akisema “inawezekanaje mtu umwambie aende na CV au kitambulisho cha Nida, kwani wakati anateuliwa haya hayakuzingatiwa?”

“Nafasi ya mkurugenzi ni nyeti sana, huyu ndiye anakwenda kusimamia mapato, katibu wa baraza la madiwani, sasa unapomteua mtu bila kumjua sijui utumishi wa umma tunauweka katika mazingira gani,” amesema

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!