Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Waziri amkingia kifua ‘boss’ wake
Habari za Siasa

Waziri amkingia kifua ‘boss’ wake

Luhaga Mpina, Waziri wa Mifugo na Uvuvi
Spread the love

LUHAGA Mpinda, Waziri wa Mifugo na Uvuvi amelalamikia watu anaodai, wanataka kumng’oa Rais John Magufuli asigombee kwenye uchaguzi mkuu 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Malwilo, Tindabuligi jimboni kwake Kisesa, Wilaya ya Meatu mkoani Simiyu, Mpina amesema watu wanaomsakama Rasi Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama chao, ni wale waliokuwa na nyadhifa za juu serikalini na kwenye chama hicho.

Mpina amesema, pamoja na watu hao kupanga mikakati ya kumkwamisha ‘boss’ wake, mikakati hiyo haitafanikiwa.

Akizungumzia mikakati hiyo Mpina amesema, viongozi hao waliwahi kupewa nafasi za juu ndani ya CCM na Serikali, lakini Watanzania walishuhudia usimamizi dhaifu wa shughuli za chama na kusababisha makundi makubwa ndani ya chama hicho.

“Walanguzi na wala rushwa waliokuwa wanaiba fedha za taifa hili wamedhibitiwa, mishahara hewa ililipwa miaka nenda rudi viongozi wakawa wanaiba mishahara hewa kana kwamba hakuna mtu aliyetakiwa kuchukua hatua… leo Mheshimiwa John Magufuli amekuja, mishahara hewa yote imekuwa historia,” amesema Mpina na kuongeza:

“Uvuvi haramu ulikuwa kila kona, samaki walikuwa hakuna Taifa lenye maziwa makubwa kuliko nchi yoyote Afrika na Dunia, Taifa lenye bahari samaki tunanunua za kutoka nje. Mheshimiwa Magufuli akasema uvuvi haramu hapana, Mpina nenda pale kakomeshe uvuvi haramu, uvuvi haramu umekoma nchi hii,” amesema.

Amesema, kwa sasa Tanzania inashuhudiwa mageuzi makubwa aliyoyafanya Rais Magufuli katika kipindi kifupi cha uongozi wake na kuwa Tanzania haitamsahau.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!