Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wazee 272 waliopigana vita Kagera waendelea kulipwa pensheni
Habari za Siasa

Wazee 272 waliopigana vita Kagera waendelea kulipwa pensheni

Spread the love

SERIKALI imesema inaendelea kuwalipa pensheni ya ulemavu wazee 272, waliopigana vita ya Kagera 1979. Anaripoti Jemimah Samwel, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamesemwa leo tarehe 9 Novemba 2023, bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Dk. Stergomena Tax, akimjibu Mbunge Viti Maalum (CCM), Fakharia Shomar, aliyehoji Serikali inatoa kauli gani kuhusu kuwasaidia walioapata ulemavu wakati wa kupigana katika vita hiyo.

Dk. Tax amesema, mbali ya wazee hao kulipwa pensheni, wanaendelea kupatiwa matibabu kwenye hospitali za jeshi, pamoja na kupata stahiki nyingine kwa mujibu wa sheria ya pensheni na viinua mgongo za mwaka 1966.

“Wengi kati ya wapiganaji hao walipewa ajira katika vyombo vya Ulinzi na Usalama hususani Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania, Jeshi la Polisi na Jeshi la Magereza. Aidha, wapo walioshindwa kuajiriwa kutokana na sababu mbalimbali,”alisema Dk. Tax.

Aidha, Dk. Tax amesema wizara yake inaendelea kufuatilia hali zao ili kuchukua hatua stahiki, huku akiwataka wazee ambao hawanufaiki na huduma hizo, kuwasilisha taarifa zao ili wasaidiwe.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

error: Content is protected !!