Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wanaofelisha watoto wapewa somo
Habari Mchanganyiko

Wanaofelisha watoto wapewa somo

Mtoto akichunga
Spread the love

WAZAZI na walezi wilayani Bahi mkoani Dodoma wametakiwa kuwekeza elimu kwa watoto wao wanaohitimu shule ya msingi na sekondari, kwa kuwaendeleza kimasomo zaidi badala ya kuwafanya warithi wa mifugo, anaandika Dany Tibason.

Pia amewataka wakulima wa wilaya hiyo kuaandaa mashamba yao kwa kuweka mbolea ili kukabiliana na mvua zinazotarajia kunyesha wakati wowote kwa mujibu wa watabiri wa hali ya hewa kwa mikoa ya kanda ya kati.

Ushauri huo umetolewa na Suleiman Yusuph, Shekhe wa wilaya ya Bahi alipokuwa akitoa mawaidha katika sala ya ljumaa iliyofanyika kwenye msikiti wa Kigwe wilayani humo.

“Wapo wazazi ambao wamekuwa wakiwataka watoto wao wafanye vibaya katika masomo yao au kuwazuia wasiende shule ili waweze kuwa wasimamizi wa mifugo, kurithi mashamba.

“Kwa ulimwengu tulionao uwezi kuwekeza kwa kumpatia mtoto elimu mifugo, jambo pekee ambalo mtoto anaweza kujivunia ni pale ambapo utaweza kumpatia elimu bora na si bora elimu” amesema Sheikh Yusuphu.

Amesema kuwa hakuna sababu ya kutowaendeleza watoto hao wanaomaliza elimu hiyo wakati serikali ya awamu ya tano imeshaomdoa michango mbalimbali ambayo ilikuwa kikwanzo katika kumwendeleza mtoto shule.

“Serikali ya awamu ya tano  michango imeondolewa ikiwemo ada kwa kuzifuta kuanzia shule za msingi hadi kidato cha nne,hivyo sioni sababu ya kumkwamisha mtoto kielimu hapa”alisema.

Akizungumza kuhusu kilimo aliwataka wakulima kuhakikisha wanaandaa mashamba hao kwa kuweka mbolea ikiwa na pamoja na kupanda mazao yanayolingana na hali ya mvua zinazonyesha kwa mikoa hiyo.

Awali akizungumza na waumini wa msikiti huo kwa upande wao aliwataka kufuata miongozo ya dini ya kiislamu siku zote za maisha yao ikiwemo kudumisha amani,upendo,umoja na mshikamano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!