Tuesday , 3 October 2023
Home Habari Mchanganyiko Wakulima Dodoma wadai kucheleweshewa fidia
Habari Mchanganyiko

Wakulima Dodoma wadai kucheleweshewa fidia

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi
Spread the love

WAKULIMA zaidi ya 70 wa kata ya Mtumba jijini Dodoma ambao maeneo ya yalipimwa na ofisi ya jiji bila kushirikishwa wanadai kitendo cha kucheleweshewa fidia zao kinawarudisha nyuma kimaendeleo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwenyekiti wa kamati ya kudai haki ya maeneo hayo, Ayubu Sanga amesema pamoja na maeneo yao yalipimwa bila wa kupewa taarifa, lakini walikubaliana walipwe fidia, cha kushajgaza hadi sasa hawajalipwa.

Amesema Oktoba 2018 ofisi ya jiji iliwaambia wananachi hao kuwa hadi kufikia Desemba mwaka jana watakuwa wamelipwa fedha hizo huku wakiambiwa watalipwa kiasi cha sh 1.5 milioni kwa hekari.

Sanga alisema kuanzia kipindi hicho hadi sasa hakuna hata mwananchi mmoja aliyelipwa fedha hizo, huku akitumia nafasi hiyo kumuomba mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi na ofisi yake kuwalipa fedha hizo ili waweze kufanya shughuli za maendeleo.

“Kata ya wananchi hao zaidi ya sabini wapo kwenye hekari 10 na wengine wanazaidi ya hekari 10, na kila hekari moja tuliambiwa tutalipwa shilingi 1.5 milioni,” alisema Sanga.

Akizungumzia malalamiko hayo afisa uhusiano wa wa jiji la Dodoma, Denis Gondwe alisema suala hilo atalifuatialia katika mamlaka husika na pindi litakapokamilika atatoa taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wawili wanaswa wakitengeneza noti bandia

Spread the loveJESHI la Polisi mkoani Songwe limewakamata watu wawili kwa tuhuza...

AfyaHabari Mchanganyiko

Chanjo mpya ya malaria Sh 5,000-10,000

Spread the loveShirika la afya la Duniani (WHO) limeridhia chanjo ya pili...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wagonjwa kiharusi waongezeka, Hospitali Mkapa yaja matibabu mapya

Spread the loveHOSPITALI ya Benjamini Mkapa kwa kushirikiana na madaktari Bingwa kutoka...

Habari Mchanganyiko

Wananchi waamua kujenga zahanati kukwepa adha kufuata huduma mbali

Spread the loveWANANCHI wa Kijiji cha Kwikerege, kilichopo katika Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!