Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wakulima Dodoma wadai kucheleweshewa fidia
Habari Mchanganyiko

Wakulima Dodoma wadai kucheleweshewa fidia

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Godwin Kunambi
Spread the love

WAKULIMA zaidi ya 70 wa kata ya Mtumba jijini Dodoma ambao maeneo ya yalipimwa na ofisi ya jiji bila kushirikishwa wanadai kitendo cha kucheleweshewa fidia zao kinawarudisha nyuma kimaendeleo. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Mwenyekiti wa kamati ya kudai haki ya maeneo hayo, Ayubu Sanga amesema pamoja na maeneo yao yalipimwa bila wa kupewa taarifa, lakini walikubaliana walipwe fidia, cha kushajgaza hadi sasa hawajalipwa.

Amesema Oktoba 2018 ofisi ya jiji iliwaambia wananachi hao kuwa hadi kufikia Desemba mwaka jana watakuwa wamelipwa fedha hizo huku wakiambiwa watalipwa kiasi cha sh 1.5 milioni kwa hekari.

Sanga alisema kuanzia kipindi hicho hadi sasa hakuna hata mwananchi mmoja aliyelipwa fedha hizo, huku akitumia nafasi hiyo kumuomba mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi na ofisi yake kuwalipa fedha hizo ili waweze kufanya shughuli za maendeleo.

“Kata ya wananchi hao zaidi ya sabini wapo kwenye hekari 10 na wengine wanazaidi ya hekari 10, na kila hekari moja tuliambiwa tutalipwa shilingi 1.5 milioni,” alisema Sanga.

Akizungumzia malalamiko hayo afisa uhusiano wa wa jiji la Dodoma, Denis Gondwe alisema suala hilo atalifuatialia katika mamlaka husika na pindi litakapokamilika atatoa taarifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!