Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kibonde azikwa makaburi ya Kinondoni, huzuni, simanzi vyatawala
Habari Mchanganyiko

Kibonde azikwa makaburi ya Kinondoni, huzuni, simanzi vyatawala

Spread the love

HATIMAYE safari ya mwisho ya aliyekuwa Mtangazaji Mahiri wa  Clouds Media Group, Ephraim Kibonde imemalizika katika Makaburi ya Kinondoni  jijini Dar es Salaam ambapo mamia ya watu ikiwemo viongozi wa kiserikali , wanasiasa na wasanii wamejitokeza kumzika mwanahabari huyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mwili wa Kibonde ulizikwa karibu na kaburi la mkewe marehemu Sara Kibonde,  leo tarehe 9 Machi 2019 majira ya kumi Alasiri .

Viongozi walioshiriki mazishi ya marehemu Kibonde ni pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne, Dk. Jakaya Kikwete, Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Suleiman Jafo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda.

Kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, Mwenyekiti wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema Zanzibar, Salum Mwalim, ni miongoni mwa wanasiasa waliojitokeza kumzika Mtangazaji huyo aliyetamba katika kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha redio cha Clouds FM.

Kabla ya mwili wa Kibonde kupumzishwa kwenye nyumba yake ya milele, aliagwa nyumbani kwao maeneo ya Mbezi Africana.

Kibonde alifariki dunia Alfajiri ya tarehe 7 Machi 2019 akiwa njiani kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Bugando jijini Mwanza kwa ajili ya kufanyiwa matibabu baada ya kusumbuliwa na presha.

Kibonde alianza kusumbuliwa na presha alipokuwa wilayani Bukoba mkoani Kagera kwenye msiba wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Vipindi na Uzalisha wa Clouds Media Group, marehemu Ruge Mutahaba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!