Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wakili Dk. Nshala aitwa kwa DCI
Habari za SiasaTangulizi

Wakili Dk. Nshala aitwa kwa DCI

Dk. Rugemeleza Nshala
Spread the love

WAKILI Rugemeleza Nshala aliyewahi kuwa Rais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) ameitwa na Ofisi ya Mkuu wa Upelelezi Kanda Maalum Dar es Salaam leo tarehe 11 Julai 2023. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea). 

Kwa mujibu wa barua iliyotolewa jana tarehe 10 Julai 2023 kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), ilimtaka wakili huyo kufika katika ofisi hiyo kutokana na kauli alizozitoa tarehe 3 Julai 2023 na kusambazwa katika vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.

Tarehe 3 Julai 2023, Dk. Nshala alitoa maoni ya kupinga makubaliano yanayohusu uwekezaji, uendelezaji na uendeshaji wa bandari uliosainiwa kati ya Serikali ya Tanzania na Dubai akieleza baadhi ya vifungu vinapingana na Katiba ya nchi.

Pia wakili huyo alidai kutishiwa kuuawa bila kufafanua ni vitisho vya namna gani hata hivyo alijinasibu kuwa yupo tayari kufa kwa kulitetea Taifa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!