Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Wabunge wataka wakaguzi wa ndani wapewe meno kudhibiti ubadhirifu
Habari za Siasa

Wabunge wataka wakaguzi wa ndani wapewe meno kudhibiti ubadhirifu

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) nchini Tanzania, Charles Kichere
Spread the love

 

SERIKALI imetakiwa kuwaongezea mamlaka wakaguzi wa ndani ili waweze kuzuia ubadhirifu na wizi wa mali ya umma unaofanywa na baadhi ya viongozi wa halmashauri nchini. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Wito huo umetolewa leo tarehe 16 Februari 2024, bungeni jijini Dodoma, na baadhi ya wabunge ambao walidai kwa sasa wakaguzi hao hawana mamlaka ya kuwashughulikia viongozi wa halmashauri kwa kuwa ni wakubwa wao (maboss).

Mbunge Viti Maalum, Agnesta Lambart, akiuliza swali kwa niaba ya mwenzake, Nusrat Hanje, amehoji kwa nini Serikali isiwahamishe wakaguzi hao katika Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), ili wawe huru katika utekelezaji wa majukumu yao.

“Serikali ina mkakati gani wa kuwajengea uwezi wa kimamlaka wakaguzi wakuu wa ndani ili kuzuia ubadhirifu na wizi wa mali za umma?,” amesema Kaiza na kuongeza:

“Moja kati ya changamoto wanazokutana nazo wakaguzi wa ndani ni hili ambalo wao wanawakagua mabosi wao jambo ambalo linapelekea ufanisi katika utendaji wao wa kazi kuwa mdogo. Lini Serikali itawaondoia chini ya wakurugenzi wa serikali za mitaa ikibidi kuwapeleka chini ya CAG?”

Naye Mbunge wa Kondoa, Ally Makoa alisema “Wizara ya Fedha haioni haja kitengo hiki cha ukaguzi wa ndani kikaondolewa kwa mkurugenzi japo kikapelekwa kwa mkuu wa wilaya ili wawe huru zaidi?”

Akiwajibu wabunge hao, Naibu Waziri wa Fedha, Hamad Chande, amesema wakaguzi hao hawawezi kuwa chini ya CAG kwa kuwa ni taasisi nyingine.

Amesema wakaguzi hao ni sehemu ya utekelezaji wa shughuli za serikali za kila kwa kukagua miradi kabla haijaanza, wakati wa kazi zinaendelea ili kuondoa changamoto zinazoweza kujitokeza. Wakati CAG ni taasisi inayokagua mradi wa serikali baada ya kukamilika ili kubaini mapungufu yaliyopo kwa ajili ya kuishauri Serikali hatua za kuchukua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za SiasaTangulizi

Samia awataka watanzania kudumisha muungano

Spread the loveRais wa Tanzania,Samia Suluhu Hassan amewataka Watanzania kuendeleza Muungano kwa...

error: Content is protected !!