Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Vyuo vikuu, michezo, ‘Form six’ kufunguliwa Juni 1
AfyaHabari za SiasaMichezoTangulizi

Vyuo vikuu, michezo, ‘Form six’ kufunguliwa Juni 1

Rais John Magufuli
Spread the love

RAIS wa Tanzania, John Magufuli ametangaza kufunguliwa kwa vyuo vyote nchini, michezo ya aina yote pamoja na wanafunzi wa kidato cha sita kuanzia tarehe 1 Juni, 2020. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais Magufuli amesema hayo leo Alhamisi tarehe 21 Mei, 2020 mara baada ya kumaliza kuwaapisha viongozi sita aliowateua hivi karibuni Ikulu ya Chamwino jijini Dodoma.

“Kasi ya maambukizi imeshuka sana, kutokana na hii hali inakwenda vizuri, tumeamua kama serikali, vyuo vyote vifunguliwe tarehe 1 Juni 2020,” amesema Rais Magufuli.

Rais Magufuli ameiagiza Wizara ya Elimu pamoja na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kujipanga katika kuhakikisha wanatengeneza mazingira mazuri kwa wanafunzi hao kuendelea na masomo.

https://youtu.be/5L_gBPViKxo

“Wizara ya elimu ipange mikakati, niwaombe na bodi ambayo inahusika na mikopo kwa wanafunzi, kuna siku tisa zijiandae ili vyuo vikifunguliwa pasije kuwa na kero nyingine,” amesema Rais Magufuli.

Tarehe 18 Machi 2020, Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu, aliagiza vyuo hivyo vifungwe kuepusha mikusanyiko, ili kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19).

Wanafunzi wa kitado cha sita wakifanya mtihani

Katika hotuba yake fupi, Rais Magufuli amesema, wanafunzi wa vyuo vikuu ni tofauti na wale wa shule za sekondari na msingi hivyo wameona waanza na vyuo kasha hali itakapokuwa nzuri watafungua na shule za sekondari na msingi.

“Kwa zile shule nyingine za sekondari na msingi zisubiri kidogo tuangalie hii ya vyuo kwa sababu ni watu wanaojitambua ni watu wazima, tujipe muda na wao baadaye tutawaoa nafasi kadri tunavyoendelea kupambana na Corona,” amesema Rais Magufuli.

Kuhusu wanafunzi wa kidato cha sita ambao walipaswa kufanya mitihani yao ya mwisho kuanzia tarehe 4 Mei, 2020, Rais Magufuli amesema nao warejee shuleni tarehe 1 Juni, 2020 kujiandaa na mitihani yao.

Ameagiza wizara ya elimu kuandaa mpango wa muda mfupi kwa ajili ya kuwaandaa wanafunzi hao kufanya mitihani yao ya mwisho ili kutokuathiri muhula wa vyuo vikuu kwa mwaka wa masomo ujayo.

Akizungumza michezo, Rais Magufuli amesema, “sina hakika kama kuna mwanamichezo aliyefariki kwa Corona Tanzania, nimeamua kuanzia tarehe 1 Juni michezo nayo ianze.”

“Ni lazima watu wafanye michezo, sasa taratibu za kuangalia na kushangilia zinaweza kupangwa lakini michezo iendelee,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Afya

Mloganzila yajipanga kupandikizaji wa ini

Spread the love  HOSPITALI ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imesema kutokana na uwekezaji uliofanywa...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

error: Content is protected !!