Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri
Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the love

VIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19 nchini, vinadaiwa kuingia mitini na fedha za mikopo kiasi cha Sh. 2.6 bilioni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Hayo yamebainishwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere, akiwasilisha ripoti ya ukaguzi kwa mwaka wa fedha wa 2022/23 kwa Rais Samia Suluhu Hassan, leo Alhamisi, jijini Dodoma.

“Katika ukaguzi wangu, nilishindwa kuthibitisha uwepo wa vikundi 851 katika halmashauri 19 vilivyopokea mikopo ya bilioni 2.6,” amesema CAG Kichere.

CAG Kichere amesema katika ukaguzi wake alioufanya kwenye mifuko miwili ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, umebaini dosari ambapo mfuko unaosimamiwa na Wizara ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI imebainika halmashauri 46 zinadai mikopo yenye thamani ya Sh. 5.7 bilioni kutoka kwa vikundi 1,334 vilivyoacha kujihusisha na shughuli za kiuchumi.

Kuhusu mfuko unaosimamiwa na Wizara ya Maendeleo ya Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, CAG Kichere amesema wamebaini kati ya 2004 hadi 2017 ulitoa mikopo kiasi cha Sh. 475.4 milioni ambayo haijarejeshwa huku mikopo yenye thamani ya Sh. 664 milioni ikitolewa bila bima.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!