Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari Vijana 854 waliofukuzwa JKT wasamehewa
Habari

Vijana 854 waliofukuzwa JKT wasamehewa

Spread the love

 

MKUU wa Majeshi Tanzania, Jenerali Venance Mabeyo amewasamehe vijana 853 wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) waliofukuzwa makambini April 12, 2021 kutokana na utovu wa nidhamu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea)

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Habari, Luteni Kanali Gervas Ilonda katika mkutano wa waandishi wa habari uliofanyika leo tarehe 5 Machi, 2022 kilichofanyika makao makuu ya jeshi, Upanga jijini Dar es Salaam.

Amesema JWTZ ina taarifa kijana mmoja kati ya wale vijana 854 waliofukuzwa amefariki na walio hai ni 853, imeamriwa vijana wote 853 warudi makambini.

Uamuzi wa kuondolewa makambini kwa vijana hao, ulitangazwa April 17, 2021 na Jenerali Mabeyo katika hafla ya kutunukiwa kamisheni kwa maafisa wapya 393 wa JWTZ na nchi rafiki.

Vijana hao walisimamishwa baada kukiuka taratibu za kijeshi kwa kuanzisha mgomo na kufanya maandamano kwenda ikulu kwa madai ya kutaka kumuona aliyekuwa rais wa wakati huo, Hayati Dk. John Pombe Magufuli.

Vijana hao walikusudia kwenda kudai kuajiriwa jeshini kama walivyoahidiwa na Hayati Magufuli, baada ya kushiriki katika ujenzi wa ofisi ya ikulu, Chamwino jijini Dodoma.

Aidha, taarifa ya kusimamishwa kwao ilieleza kwamba vijana hao walipotakiwa kusitisha mgomo huo, hawakusikia na kuendelea na mgomo wao na kuandamana, kosa ambalo jeshini linahesabika kuwa uasi.

Vijana hao ni kati ya vijana 2400 walioahidiwa kuandikishwa jeshini na walifanya uamuzi huo baada ya jeshi kuamua kuwapunguza katika kazi ya ujenzi wa Ikulu Chamwino baada ya kazi kupungua ili waende kufanya kazi katika maeneo mengine lakini wao wakapinga kwa madai wangekosa kuandikishwa jeshini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!