Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Vigogo 51 kikaangoni kwa kufuja fedha za miradi 274
Habari za Siasa

Vigogo 51 kikaangoni kwa kufuja fedha za miradi 274

Ridhiwani Kikwete
Spread the love

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete amesema katika kipindi cha Julai 2022 hadi Desemba 2023, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) iliwachukulia hatua watumishi 51 kwa matumizi mabaya ya fedha za miradi 274 ya serikali. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Kikwete ametoa kauli hiyo leo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Mbogwe, Nicodemas Maganga (CCM).

Maganga alihoji Je, Serikali inachukua hatua gani kwa watumishi wanaohusika na kutumia vibaya fedha za miradi ya Serikali?

Kikwete amesema Serikali imeendelea kuwachukulia hatua mbalimbali za kinidhamu watumishi wa umma wanaotumia vibaya fedha za miradi ya maendeleo ikiwemo kuwasimamisha kazi na kuwaanzishia mashauri ya kinidhamu.

“Mathalan, katika kipindi cha Julai 2022 hadi Desemba 2023, TAKUKURU ilifuatilia matumizi ya rasilimali za umma kwenye utekelezaji wa miradi 2,541 yenye thamani ya Sh 8.26 trilioni, ambapo miradi 467 ilibainika kuwa na mapungufu mbalimbali ikiwemo uvujaji na kutokuwa na thamani ya fedha,” amesema.

Amsema kutokana na matokeo hayo, hatua kadhaa zilichukuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Sura 329, ikiwa ni pamoja na kuanzisha uchunguzi kwa miradi 274 ambapo Watumishi 51 walichukuliwa hatua za kinidhamu

“Ofisi yangu itaendelea kufuatilia utekelezaji wa Sheria na Kanuni ili kuhakikisha kuwa Watumishi wa Umma wanazingatia miiko na maadili ya utumishi wanapotekeleza miradi ya maendeleo na pamoja majukumu mengine katika Ofisi za Umma,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

error: Content is protected !!