Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari Ummy Mwalimu asisitiza utoaji huduma bora za afya
Habari

Ummy Mwalimu asisitiza utoaji huduma bora za afya

Spread the love

 

WAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amekutana na viongozi wa idara ya kinga na kufanya mapitio ya pamoja kuhusu mafanikio, changamoto na vipaumbele katika kuimarisha huduma za kinga ili kupunguza maradhi, ulemavu. Anaripoti Danson Kaijage – Dodoma …(endelea)

Kikao hicho kimefanyika jana tarehe 17 Januari, 2022 katika ofisi za Wizara ya Afya jijini Dodoma na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Abel Makubi pamoja na Mganga Mkuu wa Serikali Dk. Aifello Sichalwe.

Katika kikao hicho, Ummy amesisitiza juu ya kuboresha utoaji huduma kwa wananchi ili kupunguza kero na malalamiko katika jamii ikiwemo huduma za lishe pamoja na mama na mtoto.

Mapitio yaliyofanywa kwenye kikao ni pamoja na ufuatiliaji na udhibiti wa magonjwa, huduma za chanjo, afya ya uzazi na mtoto, huduma za lishe, afya mazingira, elimu ya afya kwa umma.

Aidha, wamejadili mikakati mbalimbali ya mapambano dhidi ya UVIKO-19, magonjwa yaliyokuwa hayapewi kipaumbele(NTDs), malaria, kifua kikuu, ukoma na Ukimwi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

HabariSiasa

Dk. Rose Rwakatare atoa kadi 500 kila Wilaya Morogoro

Spread the loveMWENYEKITI wa Jumuiya ya Wazazi CCM Mkoa wa Morogoro, Dk...

ElimuHabari

CBE, WMA wasaini makubaliano wanafunzi kusoma wakifanyakazi

Spread the loveNAIBU Spika Musa Azzan Zungu amekipongeza Chuo cha Elimu ya...

HabariTangulizi

Dk. Slaa, Mwabukusi kuhojiwa na jeshi la Polisi Mbeya

Spread the loveJESHI la Polisi jijini Mbeya, linawashikilia kwa mahojiano Dk. Wilbroad...

HabariHabari Mchanganyiko

Kairuki Hospital Green IVF  yawanoa madaktari kuhusu upandikizaji mimba

Spread the love KITUO cha Upandikizaji Mimba cha Kairuki Hospital Green IVF...

error: Content is protected !!