Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ulega amtumbua mkurugenzi uvuvi
Habari za SiasaTangulizi

Ulega amtumbua mkurugenzi uvuvi

Stephen Lukanga
Spread the love

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega ameagiza kuondolewa katika nafasi yake Kaimu Mkurugenzi wa Uvuvi, Stephen Lukanga baada ya kushindwa kupanga na kutekeleza mikakati thabiti ya kukomesha uvuvi haramu nchini.

Prof. Mohamed Sheikh

Ameagiza nafasi hiyo apewe aliyekuwa Mkurugenzi wa Idara ya Utafiti, Mafunzo na Ugani, Prof. Mohamed Sheikh. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akimkabidhi vifaa vya uvuvi mmoja wa Wanufaika wa mkopo wa boti katika tukio la kukabidhi boti kwa wavuvi wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 28 Novemba 2023.

Waziri Ulega ametoa uamuzi huo wakati akikabidhi boti 11 zenye thamani ya Sh 1. 85 bilioni zilizotolewa na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) kwa mkopo kwa wavuvi wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 28 Novemba 2023.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdallah Ulega akikata utepe ikiwa ni ishara ya kukabidhi boti kwa wavuvi wa Dar es Salaam katika tukio la kukabidhi boti kwa wavuvi wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 28 Novemba 2023.

Ulega amefikia uamuzi huo baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wadau wa uvuvi mkoani Dar es Salaam kuhusu kukithiri kwa vitendo vya uvuvi haramu  katika ukanda Pwani hususani Dar es Salaam.

Tarehe 4 Oktoba 2023 akiwa mkoani Mwanza katika Soko la Lumumba, Ulega alimpa mwezi mmoja Kaimu Mkurugenzi huyo kuhakikisha anapanga na kutekeleza mikakati thabiti ya kukomesha uvuvi haramu nchini ambao kwa muda umekuwa ni kikwazo kwa maendeleo ya sekta ya uvuvi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!