Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko 33 wanusurika ajali ya ndege Mikumi
Habari MchanganyikoTangulizi

33 wanusurika ajali ya ndege Mikumi

Spread the love

JUMLA ya abiria 30, marubani wawili na mhudumu mmoja wamenusurika kifo katika ajali ya ndege iliyotokea leo saa 3:40 asubuhi katika Hifadhi ya Taifa Mikumi mkoani Morogoro. Anaripoti Mwandishi Wetu …(endelea).

Ndege hiyo ya kampuni ya Unity Air 5H-MJH aina ya EMBRAER 120 iliyokuwa ikitokea Zanzibar ilipata tatizo la kiufundi wakati ikitua katika kiwanja cha ndege cha Kikoboga kilichopo katika hifadhi hiyo ya Mikumi.

Taarifa iliyotolewa Afisa Uhifadhi Mwandamizi Kitengo cha Mawasiliano wa Shirika la Hifadhi za Taifa Tanzania (TANAPA), Catherine Mbena imesema juhudi kubwa zimefanywa na marubani wa ndege hiyo pamoja na maofisa katika kiwanja hicho kuhakikisha kuwa hakuna madhara yatakayotokea kutokana na ajali hiyo.

“Abiria wote 30, marubani wawili, pamoja na mhudumu wa ndege hiyo wako salama na wanaendelea na ratiba yao ya kufanya utalii hifadhini.

“Matumizi ya kiwanja pamoja na shughuli za utalii zinaendelea kama kawaida,” amesema na kuongeza kuwa;.

“TANAPA imefanya taratibu zote za kuwasiliana na idara ya uchunguzi wa ajali za ndege itiyopo Wizara ya Uchukuzi –(AAIB) kwa ajili ya taratibu zingine na uchunguzi zaidi juu ya tukio hili,” amesema.

Amesema shirika linatoa shukrani kwa kikosi cha zimamoto na uokoaji Mikumi kwa ufanisi mkubwa katika changamoto hii.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!