Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari Uhamiaji yaonya utapeli nafasi za ajira mpya
HabariHabari MchanganyikoTangulizi

Uhamiaji yaonya utapeli nafasi za ajira mpya

Spread the love

 

IDARA ya Uhamiaji nchini Tanzania, imewataka Watanzania kuwa makini dhidi ya vitendo vya utapeli vilivyoibua katika mchakato wa maombi ya nafasi za ajira 500 ilizotangaza hivi karibuni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Tahadhari hiyo imetolewa jana tarehe 14 Desemba 2022 na Msemaji Mkuu wa Idara ya Uhamiaji, Paul Mselle, akisema tangu nafasi hizo zitangazwe kumekuwepo na taarifa zenye lengo la kuwalaghai wananchi kupitia mitandao ya kijamii na baadhi kupigiwa simu na wanaotaka fedha ili wawasaidie kupata ajira hizo.

Taarifa ya Mselle imeeleza kuwa, hakuna malipo yoyote yanayohitajika kwa ajili ya waombaji kupata nafasi za ajira, hivyo wananchi wapuuze wanaowaomba fedha huku wakitakiwa kutoa taarifa kwa vyombo vya ulinzi na usalama pindi wanapopokea ujumbe unaowataka kutuma fedha ili waweze kupatiwa nafasi hizo.

“Idara inapenda kuufahamisha umma kuwa, mchakato wa ajira unaendeshwa na kusimamiwa kwa mujibu wa sheria, kanuni na taratibu za ajira kama ilivyoanishwa kwenye tangazo la ajira,” imesema taarifa ya Mselle.

Nafasi hizo za ajira zilitangazwa tarehe 11 Desemba 2022 na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji, Dk. Anna Makakala, kwa vijana wa Kitanzania waliohitimu mafunzo ya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) au Jeshi la Kujenga Uchumi (JKU).

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

error: Content is protected !!