BARAZA la Mitihani Tanzania (NECTA) leo Alhamisi limetangaza matokeo ya mtihani wa darasa la saba uliofanyika tarehe 13-14 Septemba mwaka huu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Katika matokeo hayo, jumla ya watahiniwa 1,092,960 sawa na asilimia 80.58 ya watahiniwa 1,356,296 wenye matokeo ya Mtihani wa Kumaliza Elimu ya Msingi 2023 wamefaulu ambapo wamepata madaraja ya A, B, na C.
Akitangaza matokeo hayo Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Said Mohamed amesema amefuta matokeo ya wanafunzi 31 kwa kufanya udanganyifu.
Pia amesema wanafunzi 360 ambao walipata matatizo ya kiafya na kushindwa kufanya mitihani yote au idadi kubwa ya masomo watarudia tena mwaka 2024.
Leave a comment