Monday , 5 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Tamasha la utamaduni kufanyika Dar
Habari Mchanganyiko

Tamasha la utamaduni kufanyika Dar

Kijiji cha Makumbusho
Spread the love

KAMPUNI ya masoko inayojishughulisha na ushauri na mikakati kwa wateja ZECHY Afrika imeandaa tamasha la kusheherekea utamaduni wa mtanzania (Chemichemi Canival) litakalofanyika mwezi Septemba katika kijiji cha Makumbusho jijini Dar Es Salaam, anaandika Jovina Patrick.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Lena Kimani mratibu wa tamasha amesema: “Tamasha la chemichemi linatarajia kuzinduliwa kwa kusherehekea utamaduni wa Mtanzania. Kuna matamasha mengi nchini lakini hili linalenga kusherehekea utamaduni wetu.”

Akiendelea kuongea amesema kwamba wameona uhitaji wa kufanya tamasha hilo ili kuwasaidia wanaoishi mjini kuzifahamu na kujifunza kwa ukaribu tamaduni zao kwani wengi wao hawana ukaribu na vijijini wanakotoka hali inayofamya vijana kuwa na maana hasi kuhusu utamaduni wao.

“kutokana na utandawazi mwenendo wa maisha ya watanzania wanaoishi mjini wemgi wao hawana ukaribu na vijijini wanakotoka na hili limefanya vijana wengi wa sasa kuwa na nana hasi kuhusu utamaduni wao,” anasema Lena.

Zech wanasema kuwa tamasha hilo litafanyika mara mbili kwa mwaka na hakutakuwa na kiingilio chochote ila wametoa wito kwa watakao hudhulia kuvalia nguo zao za asili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Tunduma watenga 60 milioni kujenga machinjio ya kisasa

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma Imetenga kiasi cha Tshs Miloni 60...

Habari Mchanganyiko

Bilioni 17 kujenga bandari kavu Tunduma

Spread the loveHALMASHAURI ya mji Tunduma iliyopo wilayani  Momba mkoani Songwe imepatiwa...

Habari Mchanganyiko

Bandari ya Kigoma kuongezewa uwezo wa kutoa huduma zake

Spread the love  SERIKALI kupitia mamlaka ya Bandari nchini (TPA), imewekeza takribani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kifo cha mwanafunzi UDOM: Tume yamsafisha naibu waziri

Spread the loveTUME ya Haki za Binadamu na Utawala Bora nchini (THBUB),...

error: Content is protected !!