Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Steve  Nyerere  akubali yaishe, ajiuzulu usemaji SMT
Michezo

Steve  Nyerere  akubali yaishe, ajiuzulu usemaji SMT

Spread the love

 

STEVEN Mangele maarufu Steve Nyerere ametangaza kujizulu nafasi ya Msemaji wa Shirikisho la Muziki Tanzania (SMT). Anaripoti Rhoda Kanuti, Dar es Salaam … (endelea).

Steve ametangaza uamuzi huo leo Ijumaa tarehe 25 Machi 2022 ikiwa ni siku mbili zimepita tangu Baraza la Sanaa na Taifa (Basata) kumzuia kuendelea na majukumu ya usemaji.

Basata lilimzuia Steve kuendelea na majukumu yake hayo aliyoteuliwa na viongozi wa SMT mapema mwezi huu na kuibua mpasuko miongoni mwa wasanii wa shirikisho hilo.

Mpasuko huo ulimfanya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mohamed Mchengerwa kuingilia kati na kuagiza katibu mkuu wa wizara hiyo kuitaka Basata kushughulikia mgogoro huo pamoja na kushauri inavyopaswa.

Tarehe 23 Machi 2022, Basata ilitangaza kumsimamisha Steve kuendelea na kazi hiyo hadi hapo baadaye.

Hata hivyo, leo Ijumaa akizungumza na waandishi wa habari akiwa na viongozi wa shirikisho hilo akiwemo rais wake, Ado  Novemba, katika  Ofisi za Basata  jijini Dar es Salaam, Steve ametangaza kujizulu.

“Nimejiuzulu kwa sababu sioni kama hizi kelele zina tija kwa Taifa, yanini… yanini nimeachia Taifa letu lina mambo mengi ya msingi na makubwa ya kumsapoti Rais Samia,” amesema Steve ambaye ni msanii wa vichekesho na kuigiza sauti za viongozi hususan ya Mwalimu Julius Nyerere.

Hata hivyo, amesema “tunapambana na Mama  na mtoto, Stiglers  Gorge, madarasa  na mambo mengine mengi, alafu tena tugombanie  usemaji, cheo ambacho hata mshahara wake siuoni.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC yanogesha Derby Kariakoo, Aziz Ki aibuka mchezaji bora Machi

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambayo ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!