Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Spika Tulia ampa maagizo Prof. Mkumbo
Habari za SiasaTangulizi

Spika Tulia ampa maagizo Prof. Mkumbo

Prof. Mkumbo
Spread the love

SPIKA wa Bunge, Dk.Tulia Ackson, amemuagiza Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Prof. Kitila Mkumbo, kufanya tathimini ili kujua wilaya zinazohitaji vituo vya mabasi ili Serikali ielekeze nguvu kujenga katika maeneo yenye uhitaji mkubwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Spika Tulia ametoa agizo hilo, baada ya wabunge, Joseph Tadayo (Mwanga), Ezra Chiwelesa (Biharamulo) na Victor Kawawa (Namtumbo), kuhoji lini Serikali itapelekea fedha katika majimbo yao kwa ajili ya ujenzi wa vituo (stendi) vya mabasi vya wilaya.

“Waziri wa Mipango na Uwekezaji, nadhani hili nalo ni eneo mojawapo ofisi yako ilifanyie kazi kwa maana ya mipango nchi nzima. Wapi panahitaji stendi, wapi panahitaji soko kufanya hivyo uwekezaji wa hivi kila halmashauri kujua wapi panahitaji inakuwa rahisi fedha ikipatikana inaelekezwa nguvu huko,” amesema SpikaTulia.

Awali, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, aliwajibu wabunge hao akisema Serikali inaendelea kutafuta fedha ili kujenga stendi hizo, huku akizitaka halmashauri kutenga fedha kwa ajili ya kuanza ujenzi wake kisha serikali itamalizia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Sabaya afutiwa kesi, ruksa kugombea uongozi

Spread the loveMwendesha Mashtaka Mkuu wa Serikali DPP leo Ijumaa amefuta rufaa...

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

error: Content is protected !!