Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge ataka fedha za mfuko wa jimbo ziongezwe
Habari za Siasa

Mbunge ataka fedha za mfuko wa jimbo ziongezwe

Spread the love

MBUNGE wa Wingwi, Omary Issa Kombo (CCM), ameitaka Serikali iongeze fedha za mfuko wa jimbo katika majimbo yenye uhitaji mkubwa, ikiwemo jimbo lake. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Kombo ametoa ombi hilo bungeni jijini Dodoma, leo tarehe 6 Novemba 2023, alipoihoji Serikali inatumia vigezo gani kugawa fedha hizo na lini itafanya tathimini kwa kuzingatia vigezo na ugawaji wake, ili majimbo yenye idadi kubwa ya watu yaongezewe fedha.

“Ni lini Serikali ilifanya tathimini kwa kuzingatia vigezo hivi sambamba na mgawnayo wa fedha za majimbo? Tunashuhudia baadhi ya majimbo yakipata fedha kidogo ikizingatia vigezo alivyoeleza waziri, serikali haina haja kufanya tathimini ya vigezo hivi kwa kuzingatia matokeo ya sensa ya watu na makazi ya 2022,” amesema Kombo

Akijibu maswali hayo, Naibu Waziri Ofisi ya Rais-TAMISEMI, Dk. Festo Dugange, amesema vigezo vinavyotumika katika ugawaji wa fedha za jimbo ni idadi ya watu kwa asilimia 45, mgawo wa kila jimbo (25%), kiwango cha umaskini (20%) na ukubwa wa eneo (10%).

Dk. Dugange amesema serikali inaendelea kufanya tathimini mara kwa mara ili kubaini namna nzuri ya kuboresha viwango vya ugawaji fedha za majimbo.

“Serikali inafanya tathimini mara kjwa mara kuhakikisha kwamba vinakidhi mahitaji ya fedha za mfuko wa jiumbo katika majimbo yetu, kuona namna nzuri ya kuendelea kuboresha fomula za vigezo viweze kutoka fedha. Serikali itaendelea kufanya tathimini ikionekana kuna maeneo vigezo vinatakiwa kuongezwa vitafanyika,” amesema Dk. Dugange.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

Habari za SiasaTangulizi

Mbowe: Miaka 62 ya uhuru tujenge upya mioyo yetu

Spread the loveWAKATI Tanganyika ikiadhimisha miaka 62 tangu kupata uhuru, Mwenyekiti wa...

Habari za Siasa

Rais Samia asamehe wafungwa 2,244

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amewasamehe wafungwa 2,244, huku akiwabadilishia...

error: Content is protected !!